Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Vertimas į suahilių k. - Abdullah Muchamed ir Nasir Khamis

Puslapio numeris:close

external-link copy
91 : 5

إِنَّمَا يُرِيدُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَن يُوقِعَ بَيۡنَكُمُ ٱلۡعَدَٰوَةَ وَٱلۡبَغۡضَآءَ فِي ٱلۡخَمۡرِ وَٱلۡمَيۡسِرِ وَيَصُدَّكُمۡ عَن ذِكۡرِ ٱللَّهِ وَعَنِ ٱلصَّلَوٰةِۖ فَهَلۡ أَنتُم مُّنتَهُونَ

Hakika Shetani anataka, kwa kuwapambia madhambi, kuweka baina yenu chenye kuleta uadui na chuki, kwa sababu ya kunywa pombe na kucheza kamari, na kuwaepusha na kumtaja Mwenyezi Mungu na kuswali, kwa kutokuwa na akilil katika unywaji pombe na kujishughulisha na pumbao la uchezaji kamari. Basi komekeni na hayo. info
التفاسير:

external-link copy
92 : 5

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَٱحۡذَرُواْۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na Fuateni amri, enyi Waislamu, ya kumtii Mwenyezi Mungu na kumtii Mtume Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, katika kila mnalolifanya na mnaloliacha. Na mcheni Mwenyezi Mungu na mumtunze katika hayo. Na mkikataa kufuata amri na mkayafanya mliyokatazwa, basi jueni kuwa jukumu la mjumbe wetu Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni ufikishaji ulio wazi. info
التفاسير:

external-link copy
93 : 5

لَيۡسَ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ جُنَاحٞ فِيمَا طَعِمُوٓاْ إِذَا مَا ٱتَّقَواْ وَّءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ ثُمَّ ٱتَّقَواْ وَّءَامَنُواْ ثُمَّ ٱتَّقَواْ وَّأَحۡسَنُواْۚ وَٱللَّهُ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Waumini waliokunywa pombe kabla haijaharamishwa hawana dhambi kwa kufanya hilo, iwapo wataiacha, wakajikinga na mambo yanayomkasirisha Mwenyezi Mungu na wakatanguliza matendo mema yanayoonyesha kuwa wao wanamuamini Yeye na wana hamu Mwenyezi Mungu, aliyetukuka, Awe radhi nao, kisha wakazidi kumtunza Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, na kumuamini mpaka wakawa, kwa ile yakini yao, wanamuabudu kama kwamba wao wanamuona. Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anawapenda wale ambao wamefikia kiwango cha ihsani (iḥsān) mpaka wakawa kuiamini kwao ghaibu (al-ghayb) ni kama vile wanavyoyaamini wanayoyaona.[3] info

[3]Rudia 2:3 kwa ufafanuzi wa al-ghyb.

التفاسير:

external-link copy
94 : 5

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَيَبۡلُوَنَّكُمُ ٱللَّهُ بِشَيۡءٖ مِّنَ ٱلصَّيۡدِ تَنَالُهُۥٓ أَيۡدِيكُمۡ وَرِمَاحُكُمۡ لِيَعۡلَمَ ٱللَّهُ مَن يَخَافُهُۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ فَمَنِ ٱعۡتَدَىٰ بَعۡدَ ذَٰلِكَ فَلَهُۥ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na mkafuata sheria Zake kivitendo, Mwenyezi Mungu Atawapa mtihani wa baadhi ya viwindwa vya barani, watakaokuja karibu na nyinyi kwa namna isiyo ya kawaida muweze kuwashika wadogo wao bila kutumia silaha na kuwashika wakubwa wao kwa kutumia silaha, ili Mwenyezi Mungu Awajue, ujuzi uliyofunuka wazi kwa viumbe, wale wanaomuogopa Mola wao kwa ghaibu kwa kuwa wana yakini kuwa ujuzi wa Mwenyezi Mungu kuhusu wao umekamilika, na kwa hivyo waache kuwinda wakiwa katika hali ya ihram (ihramu: kuingia kwenye ibada ya Hija au Umra). Basi yoyote mwenye kuvuka mpaka wake, baada ya maelezo haya, akafanya ujasiri wa kuwinda, na hali yeye yuko kwenye ihramu, anastahili adhabu kali. info
التفاسير:

external-link copy
95 : 5

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَقۡتُلُواْ ٱلصَّيۡدَ وَأَنتُمۡ حُرُمٞۚ وَمَن قَتَلَهُۥ مِنكُم مُّتَعَمِّدٗا فَجَزَآءٞ مِّثۡلُ مَا قَتَلَ مِنَ ٱلنَّعَمِ يَحۡكُمُ بِهِۦ ذَوَا عَدۡلٖ مِّنكُمۡ هَدۡيَۢا بَٰلِغَ ٱلۡكَعۡبَةِ أَوۡ كَفَّٰرَةٞ طَعَامُ مَسَٰكِينَ أَوۡ عَدۡلُ ذَٰلِكَ صِيَامٗا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمۡرِهِۦۗ عَفَا ٱللَّهُ عَمَّا سَلَفَۚ وَمَنۡ عَادَ فَيَنتَقِمُ ٱللَّهُ مِنۡهُۚ وَٱللَّهُ عَزِيزٞ ذُو ٱنتِقَامٍ

Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu, Mtume Wake na mkafuata sheria Zake kivitendo, msiue viwindwa wa barani na nyinyi muko kwenye ihramu ya Hija au Umra au mkawa muko ndani ya Haram. Na yoyote mwenye kuua kiwindwa yoyote kati ya viwindwa wa barani kwa kusudi, basi malipo yake ni achinje, miongoni mwa wanyama- howa: ngamia au ng’ombe au mbuzi na kondoo, anayefanana na kiwindwa huyo, baada ya waadilifu wawili kumfanyia makadirio, na amgawe kwa masikini wa eneo la Ḥarām au anunue chakula kwa thamani ya mfano wake na awagawie masikini wa eneo la Haram, kila masikini nusu pishi au afunge, badala yake, siku moja kwa kila nusu pishi ya chakula hicho. Mwenyezi Mungu Ameyapasisha malipo haya , ili mkosa apate matokeo ya kitendo chake. Na wale ambao ilitukia kwao kufanya lolote kama hilo kabla ya kuharamishwa, basi Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ashawasamehe. Na yoyote mwenye kurudia uhalifu huo kwa kusudi, baada ya kuharamishwa, huyo amejihatarisha kupata mateso ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu katika mamlaka Yake, na miongoni mwa enzi Yake ni kuwa Yeye atamtesa anayemuasi Akitaka, hakuna chenye kumzuia kufanya hivyo. info
التفاسير: