Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Vertimas į suahilių k. - Abdullah Muchamed ir Nasir Khamis

Puslapio numeris:close

external-link copy
105 : 17

وَبِٱلۡحَقِّ أَنزَلۡنَٰهُ وَبِٱلۡحَقِّ نَزَلَۗ وَمَآ أَرۡسَلۡنَٰكَ إِلَّا مُبَشِّرٗا وَنَذِيرٗا

Na tumemteremshia Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, hii Qur’ani ili kuwaamrisha waja, kuwakataza, kuwalipa mema na kuwaadhibu; na imeteremka kwa ukweli, uadilifu na utunzi isibadilishwe na isigeuzwe. Na hatukukutumiliza wewe, ewe Mtume, isipokuwa ni uwabashirie Pepo waliotii na uwatishe na Moto walioasi na kukanusha. info
التفاسير:

external-link copy
106 : 17

وَقُرۡءَانٗا فَرَقۡنَٰهُ لِتَقۡرَأَهُۥ عَلَى ٱلنَّاسِ عَلَىٰ مُكۡثٖ وَنَزَّلۡنَٰهُ تَنزِيلٗا

Na tumekuteremshia, ewe Mtume, Qur’ani tuliyoieleza, tukaipanga na kuifafanua ikawa ni yenye kutenganisha baina ya uongofu na upotevu na ukweli na ubatilifu, ili upate kuwasomea watu kwa umakinifu na upole; na tumeiteremsha mafungu-mafungu kidogo-kidogo kulingana na matukio ya wakati na mahitaji yake. info
التفاسير:

external-link copy
107 : 17

قُلۡ ءَامِنُواْ بِهِۦٓ أَوۡ لَا تُؤۡمِنُوٓاْۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ مِن قَبۡلِهِۦٓ إِذَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ يَخِرُّونَۤ لِلۡأَذۡقَانِۤ سُجَّدٗاۤ

Sema, ewe Mtume, uwaambie hawa wakanushaji, «Iaminini Qur’ani au msiiamini, kwani kuiamini kwenu hakuiongezei ukamilifu, na kuikanusha kwenu hakuifanyi iwe na upungufu, kwani wanavyuoni waliopewa Vitabu vilivyotangulia kabla ya Qur’ani na wakajua uhakika wa wahyi, wanaposomewa Qur’ani wananyenyekea na wanamsujudia Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kwa nyuso zao kwa kumtukuza na kwa kumshukuru. info
التفاسير:

external-link copy
108 : 17

وَيَقُولُونَ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِن كَانَ وَعۡدُ رَبِّنَا لَمَفۡعُولٗا

Na wanasema, hawa waliopewa ujuzi, wanapoisikia Qur’ani, «Kuepukana na kutakasika ni kwa Mola wetu na kila sifa wanazompa washirikina; halikuwa agizo la Mwenyezi Mungu Aliyetukuka isipokuwa ni lenye kutukia kikweli.» info
التفاسير:

external-link copy
109 : 17

وَيَخِرُّونَ لِلۡأَذۡقَانِ يَبۡكُونَ وَيَزِيدُهُمۡ خُشُوعٗا۩

Na hapo hawa wanapomoka hali ya kusujudu kwa nyuso zao, huku wakilia kwa kuathirika na mawaidha ya Qur’ani. Na kule kuisikia Qur’ani na mawaidha yake kunawafanya wazidi kuinyenyekea amri ya Mwenyezi Mungu na kuunyenyekea uweza Wake mkubwa. info
التفاسير:

external-link copy
110 : 17

قُلِ ٱدۡعُواْ ٱللَّهَ أَوِ ٱدۡعُواْ ٱلرَّحۡمَٰنَۖ أَيّٗا مَّا تَدۡعُواْ فَلَهُ ٱلۡأَسۡمَآءُ ٱلۡحُسۡنَىٰۚ وَلَا تَجۡهَرۡ بِصَلَاتِكَ وَلَا تُخَافِتۡ بِهَا وَٱبۡتَغِ بَيۡنَ ذَٰلِكَ سَبِيلٗا

Sema, ewe Mtume, kuwaambia washirikina wa watu wako waliokupinga kutumia kwako neno la Yā Allāh , Yā Raḥmān, katika maombi, «Muombeni Allāh (Mwenyezi Mungu) au muombeni Raḥmān (Mwingi wa rehema), kwani kwa majina yoyote yake mkimuomba huwa mnamuomba Mola Mmoja, kwa kuwa majina Yake yote ni mazuri. Wala usidhihirishe kisomo katika Swala yako wakakusikia washirikina, wala usisome kwa siri wasikusikie masahaba zako, na uwe kati na kati baina ya kudhihirisha na kusirisha.» info
التفاسير:

external-link copy
111 : 17

وَقُلِ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي لَمۡ يَتَّخِذۡ وَلَدٗا وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ شَرِيكٞ فِي ٱلۡمُلۡكِ وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ وَلِيّٞ مِّنَ ٱلذُّلِّۖ وَكَبِّرۡهُ تَكۡبِيرَۢا

Na useme, «Shukrani zote ni za Mwenyezi Mungu, ukamilifu na sifa njema ni Zake, Aliyeepukana na mwana na mshirika katika uungu Wake. Na Mwenyezi Mungu Hana msaidizi yoyote kati ya viumbe vyake, Yeye Ndiye Mkwasi na Ndiye Mwenye nguvu., na wao ndio mafukara wanaomhitajia.» Na umtukuze matukuzo yaliyotimu, kwa kumsifu, kumuabudu Peke Yake bila ya mshirika, na kumtakasia Dini yote.» info
التفاسير: