[1] Hapa Mwenyezi Mugnu aliufananisha uwongofu aliowaongoza kwao waja wake, na mvua. Kwa sababu, nyoyo huhuishwa kwa uwongofu, kama vile ardhi huhuishwa na mvua. Na fungu la wanafiki katika uwongofu huo ni kama fungu la yule ambaye hakupata katika mvua isipokuwa giza, radi na umeme, wala hana fungu zaidi ya hayo katika yale yaliyokusudiwa kutoka kwa mvua hiyo kama vile uhai wa nchi, watu, miti na wanyama. (Tafsir Ibn Al-Qayyim)