[1] Kuiharibu ni kwa aina mbili: kihisia na kimaana. Ama kuiharibu kwa kihisia ni kuibomoa, kuiharibu, na kuichafua. Nako kuharibu kwa kimaana ni kuwazuia wale wanaolitaja jina la Mwenyezi Mungu ndani yake (Tafsir Assa'dii).
[1] Katika Aya hii, kuna kukanusha Mwenyezi Mungu kuwa na mwana. Kwa sababu, Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake bila ya mfano wa awali. Basi hakuna hata mmoja katika viumbe hao anayestahiki kuwa mwanawe, bali kila kitu humo ni waja (viumbe) wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. (Tafsir Attahrir wa Attanwir cha Ibn 'Aashur)
[1] Na kauli yake, "Na anapotaka jambo, basi Yeye kwa hakika huliambia tu: Kuwa! Nalo huwa," ni jawabu kwa dhana potofu ya Wakristo kwamba Mwenyezi Mungu ana mwana; ati kwa sababu kupatikana kwa Masihi bila ya baba ni dalili ya kuwa yeye ni mwana wa Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo, Mwenyezi Mungu Mtukufu akaweka wazi kwamba kuunda vitu bila ya kutokana na kitu ni ajabu zaidi kuliko hilo la Masihi (kuwa na mama bila baba). (Tafsir Attahrir wa Attanwir cha Ibn 'Aashur)