ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
24 : 48

وَهُوَ ٱلَّذِي كَفَّ أَيۡدِيَهُمۡ عَنكُمۡ وَأَيۡدِيَكُمۡ عَنۡهُم بِبَطۡنِ مَكَّةَ مِنۢ بَعۡدِ أَنۡ أَظۡفَرَكُمۡ عَلَيۡهِمۡۚ وَكَانَ ٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرًا

Na Yeye Ndiye Aliyeizuia mikono ya washirikina isiwafikie nyinyi, na mikono yenu isiwafikie wao katika bonde la Makkah baada nyinyi kuwaweza wao wakawa chini ya mamlaka yanu. (washirikina hawa ndio wale waliotoka kuishambulia kambi ya askari wa Mtume wa Mwenyezi Mungu , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hapo Ḥudaybiyah, Waislamu wakawakamata kisha wakawaachilia wasiwaue, na walikuwa ni kiasi cha wanaume themanini.) Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona matendo yenu, hakuna chochote kinafichamana Kwake. info
التفاسير:

external-link copy
25 : 48

هُمُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَصَدُّوكُمۡ عَنِ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ وَٱلۡهَدۡيَ مَعۡكُوفًا أَن يَبۡلُغَ مَحِلَّهُۥۚ وَلَوۡلَا رِجَالٞ مُّؤۡمِنُونَ وَنِسَآءٞ مُّؤۡمِنَٰتٞ لَّمۡ تَعۡلَمُوهُمۡ أَن تَطَـُٔوهُمۡ فَتُصِيبَكُم مِّنۡهُم مَّعَرَّةُۢ بِغَيۡرِ عِلۡمٖۖ لِّيُدۡخِلَ ٱللَّهُ فِي رَحۡمَتِهِۦ مَن يَشَآءُۚ لَوۡ تَزَيَّلُواْ لَعَذَّبۡنَا ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡهُمۡ عَذَابًا أَلِيمًا

Makafiri wa Kikureshi ndio waliokataa kumpwekesha Mwenyezi Mungu, wakawazuia nyinyi, Siku ya Ḥudaybiyah, kuingia Msikiti wa al-Ḥarām, wakakataza wanyama na wakawafunga wasifike mahali pa wao kuchinjwa, napo ni Ḥarām. Na lau si wanaume Waumini walio wanyonge na wanawake Waumini msiowajua, walio kati ya hawa makafiri wa Makkah, wanaoificha Imani yao kwa kuzichelea nafsi zao, msije mkawakanyaga kwa jeshi lenu mkawaua, mkapata dhambi, aibu na gharama kwa mauaji hayo bila kujua, tungaliwapa nyinyi uwezo juu yao, ili Mwenyezi Mungu Apate kumtia kwenye rehema Zake Anayemtaka kwa kumpa neema ya kuamini baada ya kukanusha. Lau hawa Waumini wa kiume na Waumini wa kike wangalitenganika na washirikina wa Makkah na wakajitoa kati yao, tungaliwaadhibu wale waliokufuru na kukanusha miongoni mwao adhabu yenye uchungu na kuumiza. info
التفاسير:

external-link copy
26 : 48

إِذۡ جَعَلَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلۡحَمِيَّةَ حَمِيَّةَ ٱلۡجَٰهِلِيَّةِ فَأَنزَلَ ٱللَّهُ سَكِينَتَهُۥ عَلَىٰ رَسُولِهِۦ وَعَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَأَلۡزَمَهُمۡ كَلِمَةَ ٱلتَّقۡوَىٰ وَكَانُوٓاْ أَحَقَّ بِهَا وَأَهۡلَهَاۚ وَكَانَ ٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٗا

Pindi wale waliokanusha walipoingiza ndani ya nyoyo zao ghera, ghera za watu wa zama za ujinga, ili wasikubali utume wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na miongoni mwa hayo ni kule kukataa kwao kwandika «Bi ism Allāh al-Raḥmān al-Raḥīm» katika mapatano ya Ḥudaybiyah, na wakakataa kuandika, «Haya ndiyo yale aliyoyapitisha Muhammad, Mtume wa Mwenyezi Mungu.» Na Mwenyezi Mungu Akamteremshia utulivu Mtume Wake na Waumini pamoja na yeye, Akawathibitishia neno «Lā ilāha illā Allāh» ambalo ndio kichwa cha ya kila uchamungu. Na Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Waumini pamoja na yeye ndio wanaostahiki zaidi neno la uchamungu kuliko washirikina. Na hivyo ndivyo walivyokuwa, walistahiki neno hili na sio washirikina. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa ujuzi wa kila kitu, hakuna kitu chochote kinachofichamana Kwake. info
التفاسير:

external-link copy
27 : 48

لَّقَدۡ صَدَقَ ٱللَّهُ رَسُولَهُ ٱلرُّءۡيَا بِٱلۡحَقِّۖ لَتَدۡخُلُنَّ ٱلۡمَسۡجِدَ ٱلۡحَرَامَ إِن شَآءَ ٱللَّهُ ءَامِنِينَ مُحَلِّقِينَ رُءُوسَكُمۡ وَمُقَصِّرِينَ لَا تَخَافُونَۖ فَعَلِمَ مَا لَمۡ تَعۡلَمُواْ فَجَعَلَ مِن دُونِ ذَٰلِكَ فَتۡحٗا قَرِيبًا

Kwa hakika Mwenyezi Mungu Alimsadikishia Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ndoto yake aliyomuotesha kwa haki kwamba utaingia, wewe na Maswahaba wako, Nyumba takatifu ya Mwenyezi Mungu hali ya kuwa mko katika amani, hamuwaogopi watu wa ushirikina, hali ya kuwa mnanyoa vichwa vyenu na mnapunguza. Mwenyezi Mungu Alijua kheri na maslahi ya kuwaepusha nyinyi na Makkah mwaka wenu huo na kuingia huko baadae, msiyoyajua nyinyi, na Akajaalia, kabla ya kuingia kwenu Makkah mliyoahidiwa, ufunguzi wa karibu, nao ni mapatano ya amani ya Ḥudaybiyah na ufunguzi wa Khaybar. info
التفاسير:

external-link copy
28 : 48

هُوَ ٱلَّذِيٓ أَرۡسَلَ رَسُولَهُۥ بِٱلۡهُدَىٰ وَدِينِ ٱلۡحَقِّ لِيُظۡهِرَهُۥ عَلَى ٱلدِّينِ كُلِّهِۦۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدٗا

Yeye Ndiye Aliyemtumiliza Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa ubainufu ulio wazi na Dini ya Uislamu, ili aifanye kuwa juu ya mila zote. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa ni shahidi kwamba Yeye ni Mwenye kukupa ushindi na kuidhihirisha Dini yako juu ya kila dini. info
التفاسير: