ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
21 : 41

وَقَالُواْ لِجُلُودِهِمۡ لِمَ شَهِدتُّمۡ عَلَيۡنَاۖ قَالُوٓاْ أَنطَقَنَا ٱللَّهُ ٱلَّذِيٓ أَنطَقَ كُلَّ شَيۡءٖۚ وَهُوَ خَلَقَكُمۡ أَوَّلَ مَرَّةٖ وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Na watasema hao watakaokusanywa kupelekwa Motoni miongoni mwa maadui wa Mwenyezi Mungu kuziambia ngozi zao wakizilaumu, «Kwa nini mmetoa ushahidi dhidi yetu?» Na hapo ngozi zao ziwajibu, «Ametutamsha Mwenyezi Mungu Ambaye Amekitamsha kila kitu, na Yeye Ndiye Aliyewaumba nyinyi mara ya kwanza na hamkuwa ni chochote, na kwake Yeye Ndio mwisho wenu baada ya kufa ili mhesabiwe na mlipwe.» info
التفاسير:

external-link copy
22 : 41

وَمَا كُنتُمۡ تَسۡتَتِرُونَ أَن يَشۡهَدَ عَلَيۡكُمۡ سَمۡعُكُمۡ وَلَآ أَبۡصَٰرُكُمۡ وَلَا جُلُودُكُمۡ وَلَٰكِن ظَنَنتُمۡ أَنَّ ٱللَّهَ لَا يَعۡلَمُ كَثِيرٗا مِّمَّا تَعۡمَلُونَ

Na hamkuwa mkijificha mlipokuwa mkitenda maasia kwa kuogopa yasije masikio yenu wala macho yenu wala ngozi zenu yakatoa ushahidi dhidi yenu Siku ya Kiyama, lakini mlidhani , kwa kufanya maasia kwenu, kuwa Mwenyezi Mungu hajui mengi kuhusu matendo yenu ambayo kwayo mnamuasi Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
23 : 41

وَذَٰلِكُمۡ ظَنُّكُمُ ٱلَّذِي ظَنَنتُم بِرَبِّكُمۡ أَرۡدَىٰكُمۡ فَأَصۡبَحۡتُم مِّنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

Hiyo ndiyo dhana yenu mbovu ambayo mliidhania kwa Mola wenu; imewaangamiza na kuwatia Motoni, ndipo mkawa Leo ni miongoni mwa wale waliopata hasara nafsi zao na ya watu wao. info
التفاسير:

external-link copy
24 : 41

فَإِن يَصۡبِرُواْ فَٱلنَّارُ مَثۡوٗى لَّهُمۡۖ وَإِن يَسۡتَعۡتِبُواْ فَمَا هُم مِّنَ ٱلۡمُعۡتَبِينَ

Wakivumilia adhabu, basi Moto ndio makazi yao, na wakiomba kurejea duniani waanze kufanya amali njema huko, hawatajibiwa ombi hilo wala hazitakubaliwa nyudhuru zao. info
التفاسير:

external-link copy
25 : 41

۞ وَقَيَّضۡنَا لَهُمۡ قُرَنَآءَ فَزَيَّنُواْ لَهُم مَّا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡ وَحَقَّ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقَوۡلُ فِيٓ أُمَمٖ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِهِم مِّنَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ خَٰسِرِينَ

Na tuliwawekea hawa madhalimu wenye kukanusha marafiki wabaya miongoni mwa Mashetani wa kibinadamu na wa kijini, wakawapambia matendo yao machafu duniani, wakawaita kwenye ladha zake na matamanio yake ya haramu, na wakawapambia wao yaliyo nyuma yao katika mambo ya Akhera wakawasahaulisha wasiikumbuke, na wakawalingania wakatae Marejeo (ya Kiyama). Na kwa hjvyo walistahili kuingia Motoni wawe miongoni mwa wale makafiri wa ummah waliopita wa kijini na wa kibinadamu. Wao walikuwa wamepata hasara ya matendo yao duniani na hasara ya nafsi zao na watu wao Siku ya Kiyama. info
التفاسير:

external-link copy
26 : 41

وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَا تَسۡمَعُواْ لِهَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ وَٱلۡغَوۡاْ فِيهِ لَعَلَّكُمۡ تَغۡلِبُونَ

Na makafiri walisema wakiambiana wao kwa wao wakiusiana baina yao, «Msiisikilize hii Qur’ani wala msiiandame wala msizifuate amri zake. Na ziinueni juu sauti zenu kwa kelele, kupiga mbinja na kumfanya Muhammad achanganyikiwe anaposoma Qur’ani, huenda mkamshinda akaacha kusoma na kwa hivyo tukapata ushindi juu yake.» info
التفاسير:

external-link copy
27 : 41

فَلَنُذِيقَنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ عَذَابٗا شَدِيدٗا وَلَنَجۡزِيَنَّهُمۡ أَسۡوَأَ ٱلَّذِي كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Basi Tutawaonjesha, tena tutawaonjesha, wale waliosema neno hili adhabu kali, duniani na Akhera, na tutawalipa, tena tutawalipa, mabaya zaidi ya makosa waliokuwa wakiyafanya. info
التفاسير:

external-link copy
28 : 41

ذَٰلِكَ جَزَآءُ أَعۡدَآءِ ٱللَّهِ ٱلنَّارُۖ لَهُمۡ فِيهَا دَارُ ٱلۡخُلۡدِ جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَجۡحَدُونَ

Malipo haya ambayo watalipwa waliokufuru ni malipo ya maadui wa Mwenyezi Mungu, nayo ni Moto utakaokuwa ni nyumba yao ya kukaa daima milele, ukiwa ni malipo ya wale waliokuwa wakizikanusha hoja zetu na dalili zetu. Na aya hii inatolea ushahidi ukubwa wa kosa la mwenye kuwapotosha watu na Qur’ani tukufu na kuwazuia wasiizingatie wala wasijiongoze nayo kwa njia yoyote iwayo. info
التفاسير:

external-link copy
29 : 41

وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ رَبَّنَآ أَرِنَا ٱلَّذَيۡنِ أَضَلَّانَا مِنَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِ نَجۡعَلۡهُمَا تَحۡتَ أَقۡدَامِنَا لِيَكُونَا مِنَ ٱلۡأَسۡفَلِينَ

Na watasema wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wao wako Motoni, «Mola wetu! Tuonyeshe mapote mawili yaliyotupoteza miongoni mwa majini na binadamu ili tuyaweke chini ya nyayo zetu yapate kuwa sehemu ya chini kabisa ya Moto.» info
التفاسير: