ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
19 : 35

وَمَا يَسۡتَوِي ٱلۡأَعۡمَىٰ وَٱلۡبَصِيرُ

Na kipofu asiyeiona Dini ya Mwenyezi Mungu halingani na yule mwenye kuona ambaye anaiona njia ya haki na anaifuata. info
التفاسير:

external-link copy
20 : 35

وَلَا ٱلظُّلُمَٰتُ وَلَا ٱلنُّورُ

Na giza la ukafiri halilingani na mwangaza wa Imani, info
التفاسير:

external-link copy
21 : 35

وَلَا ٱلظِّلُّ وَلَا ٱلۡحَرُورُ

wala kivuli hakilingani na upepo wa joto. info
التفاسير:

external-link copy
22 : 35

وَمَا يَسۡتَوِي ٱلۡأَحۡيَآءُ وَلَا ٱلۡأَمۡوَٰتُۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُسۡمِعُ مَن يَشَآءُۖ وَمَآ أَنتَ بِمُسۡمِعٖ مَّن فِي ٱلۡقُبُورِ

Na wale waliohuika nyoyo kwa kukuamini hawalingani na wale waliokufa nyoyo kwa kukanusha. Hakika Mwenyezi Mungu Anamsikilizisha Anayemtaka asikie kwa kufahamu na kukubali. Na wewe, ewe Mtume, si mwenye kuwasikilizisha walio ndani ya makaburi. Na kama usivyoweza kuwasikilizisha wafu makaburini mwao, pia hutawasikilizisha hawa makafiri kwa kuwa nyoyo zao zimekufa. info
التفاسير:

external-link copy
23 : 35

إِنۡ أَنتَ إِلَّا نَذِيرٌ

Wewe hukuwa isipokuwa ni mwenye kuwaonya ghadhabu za Mwenyezi Mungu na mateso Yake. info
التفاسير:

external-link copy
24 : 35

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ بَشِيرٗا وَنَذِيرٗاۚ وَإِن مِّنۡ أُمَّةٍ إِلَّا خَلَا فِيهَا نَذِيرٞ

Sisi tumekutumiliza kwa haki, nayo ni kumuamini Mwenyezi Mungu na Sheria za Dini, hali ya kuwapa bishara ya Pepo wale wenye kukuamini na wakaufuata uongofu wako kivitendo, na hali ya kuwaonya Moto wale waliokukanusha na wakakuasi. Na hakuna taifa lolote la watu isipokuwa limejiwa na muonyaji wa kuwaonya mwisho mbaya wa ukafiri wao na upotevu wao. info
التفاسير:

external-link copy
25 : 35

وَإِن يُكَذِّبُوكَ فَقَدۡ كَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَبِٱلزُّبُرِ وَبِٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُنِيرِ

Na wanapokukanusha washirikina hawa , basi wale waliopita kabla yao waliwakanusha Mitume wao ambao waliwajia na miujiza iliyo wazi yenye kutolea ushahidi unabii wao, na waliwajia na Vitabu, ambavyo ndani yake zimekusanywa hukumu nyingi, na (waliwajia na) Kitabu chenye kutoa mwangaza chenye kubainisha njia ya kheri na shari. info
التفاسير:

external-link copy
26 : 35

ثُمَّ أَخَذۡتُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۖ فَكَيۡفَ كَانَ نَكِيرِ

Kisha nikawakamata wale waliokanusha na kuwapa aina mbalimbali za adhabu. Basi angalia kulikuwa namna gani kukataa kwangu matendo yao na kule kuwashukia wao mateso yangu? info
التفاسير:

external-link copy
27 : 35

أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ أَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَخۡرَجۡنَا بِهِۦ ثَمَرَٰتٖ مُّخۡتَلِفًا أَلۡوَٰنُهَاۚ وَمِنَ ٱلۡجِبَالِ جُدَدُۢ بِيضٞ وَحُمۡرٞ مُّخۡتَلِفٌ أَلۡوَٰنُهَا وَغَرَابِيبُ سُودٞ

Kwani huoni kwamba Mwenyezi Mungu Ameteremsha kutoka juu maji, tukainywesha kwayo miti iliyo ardhini, tukatoa kwenye miti hiyo matunda yenye rangi tofauti, miongoni mwazo ni nyekundu na miongoni mwazo nyeusi na manjano na zisizokuwa hizo? Na tumeumba majabalini njia zenye rangi tofauti, nyeupe na nyekundu. Na tumeumba miongoni mwa majabali, majabali meusi sana. info
التفاسير:

external-link copy
28 : 35

وَمِنَ ٱلنَّاسِ وَٱلدَّوَآبِّ وَٱلۡأَنۡعَٰمِ مُخۡتَلِفٌ أَلۡوَٰنُهُۥ كَذَٰلِكَۗ إِنَّمَا يَخۡشَى ٱللَّهَ مِنۡ عِبَادِهِ ٱلۡعُلَمَٰٓؤُاْۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ غَفُورٌ

Na miongoni mwa watu na wanyama, ngamia, ng’ombe, mbuzi na kondoo tumeumba wakiwa rangi tofauti vilevile. Kati ya hao kuna wekundu, weupe weusi na wenye rangi nyinginezo, kama vile kutofautiana rangi za matunda na majabali. Hakika wanaomcha Mwenyezi Mungu na kujikinga na mateso Yake kwa kumtii na kujiepusha kumuasi ni wale wanaomjua Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake,sifa Zake na Sheria Zake, na uweza Wake juu ya kila kitu ambao miongoni mwavyo ni kutofautiana viumbe hivi pamoja na kuwa sababu yake ni moja, na wanayatia akilini yaliyomo ndani ya mawaidha na mazingatio. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mshindi Mwenye nguvu Asiyeshindwa, Mwingi wa kusamehe Anawapa malipo mema watiifu, na Anawasamehe. info
التفاسير:

external-link copy
29 : 35

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَتۡلُونَ كِتَٰبَ ٱللَّهِ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَأَنفَقُواْ مِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ سِرّٗا وَعَلَانِيَةٗ يَرۡجُونَ تِجَٰرَةٗ لَّن تَبُورَ

Hakika ya wale wanaosoma Qur’ani na wakaifanyia kazi, wakaendelea daima kuswali kwa nyakati zake na wakatumia kile tulichowaruzuku miongoni mwa aina ya matumizi ya lazima na ya yanayopendekezwa, kwa siri na kwa dhahiri, hao wana matumaini kwa hayo kufanya biashara isiyoenda na isiyoanguka, nayo ni kuridhiwa na Mola wao na kufaulu kupata malipo mema mengi Yake. info
التفاسير:

external-link copy
30 : 35

لِيُوَفِّيَهُمۡ أُجُورَهُمۡ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضۡلِهِۦٓۚ إِنَّهُۥ غَفُورٞ شَكُورٞ

Ili Awatimizie Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, malipo mema ya matendo yao yakiwa kamili bila kupunguzwa, na wataongezewa mema kwa fadhila Zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Msamehefu sana wa makosa yao, ni Mwingi wa shukrani kwa mema yao, Atawalipa kwa mema hayo malipo mazuri mengi. info
التفاسير: