Ninaapa kwa pepo zinazo timua mawingu, zikayasukuma kwa nguvu, huku zikibeba mizigo mizito ya maji, zikawa zinakwenda kwa wepesi kwa amri ya Mwenyezi Mungu, zikawa zinagawanya riziki kwa ampendaye Mwenyezi Mungu.
التفاسير:
2:51
فَٱلۡحَٰمِلَٰتِ وِقۡرٗا
Na zinazo beba mizigo!
Huku zikibeba mizigo mizito ya maji.
التفاسير:
3:51
فَٱلۡجَٰرِيَٰتِ يُسۡرٗا
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
Zikawa zinakwenda kwa wepesi kwa amri ya Mwenyezi Mungu.
التفاسير:
4:51
فَٱلۡمُقَسِّمَٰتِ أَمۡرًا
Na zinazo gawanya kwa amri!
Zikawa zinagawanya riziki kwa ampendaye Mwenyezi Mungu.
التفاسير:
5:51
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٞ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli!
Hakika hayo mnayo ahidiwa, nayo ya kufufuliwa na mengineyo, ni hakika ya kweli itakayo tokea.
التفاسير:
6:51
وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٞ
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
Na kwamba kwa yakini malipo kwa vitendo vyenu yatakuwa tu hapana hivi wala hivi.