クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany

external-link copy
50 : 5

أَفَحُكۡمَ ٱلۡجَٰهِلِيَّةِ يَبۡغُونَۚ وَمَنۡ أَحۡسَنُ مِنَ ٱللَّهِ حُكۡمٗا لِّقَوۡمٖ يُوقِنُونَ

Je, wao wanataka hukumu za Kijahiliya? Na nani aliye mwema zaidi katika kuhukumu kuliko Mwenyezi Mungu kwa watu wenye yakini? info

Je, hao wanao kataa amri na makatazo ya Mwenyezi Mungu wanataka wahukumiwe kwa hukumu ya Kijahiliya, ya kijinga, ya kabla ya kufika Uislamu, kulipo kuwa hapana uadilifu, bali matamanio ya nafsi tu ndiyo yliyo kuwa yakihukumu, na mapendeleo na udanganyifu ndio msingi wa hukumu? Huo ndio mwendo wa watu wa zama za Kijahiliya! Yuko aliye bora kuliko Mwenyezi Mungu kuhukumu watu wenye kuyakinika na Sharia na wenye kunyenyekea Haki? Kwa hakika hao ndio wanao tambua ubora wa hukumu za Mwenyezi Mungu.

التفاسير: