クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis

ページ番号:close

external-link copy
76 : 17

وَإِن كَادُواْ لَيَسۡتَفِزُّونَكَ مِنَ ٱلۡأَرۡضِ لِيُخۡرِجُوكَ مِنۡهَاۖ وَإِذٗا لَّا يَلۡبَثُونَ خِلَٰفَكَ إِلَّا قَلِيلٗا

Na makafiri walikaribia kukutoa Makkah kwa kukukera, na lau walikutoa huko hawangalikaa huko baada yako isipokuwa muda mchache, hadi iwashukie adhabu ya ulimwenguni.[6] info

[6]Tafsiri ya aya hii yategemea moja ya sababu zilizotajwa za kuteremka kwake, nayo ni kuwa makafiri wa kikureshi walitaka kumtoa Mtume (s.a.w) kwenye mji, Mwenyezi Mungu Akawaonya kwa aya hii na kwamba wao lau walimtoa hawangalikaa kwenye mji wa Makkah baada yao isipokuwa muda mchache. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, kwani haukupita muda mrefu baada ya kugura kwa Mtume (s.a.w) kwenda Madīnah mpaka Mwenyezi Mungu Akawakusanya na wao hapo Badr, hapo wakubwa wao wakauawa na wengine kutekwa. Tazama Ibn Kathīr katika kufasiri aya hii.

التفاسير:

external-link copy
77 : 17

سُنَّةَ مَن قَدۡ أَرۡسَلۡنَا قَبۡلَكَ مِن رُّسُلِنَاۖ وَلَا تَجِدُ لِسُنَّتِنَا تَحۡوِيلًا

Huo ndio mwendo uliowekwa na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, katika kuwaangamiza watu wanaomtoa Mtume wao kutoka kwao, na hutapata mabidiliko kwenye mwendo wetu, kwani hatuendi kinyume na ahadi yetu. info
التفاسير:

external-link copy
78 : 17

أَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ لِدُلُوكِ ٱلشَّمۡسِ إِلَىٰ غَسَقِ ٱلَّيۡلِ وَقُرۡءَانَ ٱلۡفَجۡرِۖ إِنَّ قُرۡءَانَ ٱلۡفَجۡرِ كَانَ مَشۡهُودٗا

Simamisha Swala itimie kuanzia kipindi cha kupinduka jua wakati wa mchana mpaka kipindi cha usiku. Inaingia hapa Swala ya Adhuhuri, Alasiri, Magharibi na Isha. Na simamisha Swala ya Alfajiri na urefushe kisomo chake, kwani Swala ya Alfajiri inahudhuriwa na Malaika wa usiku na Malaika wa mchana. info
التفاسير:

external-link copy
79 : 17

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَتَهَجَّدۡ بِهِۦ نَافِلَةٗ لَّكَ عَسَىٰٓ أَن يَبۡعَثَكَ رَبُّكَ مَقَامٗا مَّحۡمُودٗا

Na inuka, ewe Nabii, kutoka kwenye usingizi sehemu ya usiku, usome Qur’ani katika Swala ya usiku, ipate kuwa, hiyo Swala ya usiku, ni nyongeza kwako katika utukufu wa cheo na kupandishiwa daraja. Huenda Mwenyezi Mungu Akakuleta uwe ni mwenye kuwashufaia watu Siku ya Kiyama, ili Mwenyezi Mungu Awarehemu kwa kuwaondolea waliokuwa nayo, na usimame kisimamo ambacho watakushukuru kwacho wa mwanzo na wa mwisho. info
التفاسير:

external-link copy
80 : 17

وَقُل رَّبِّ أَدۡخِلۡنِي مُدۡخَلَ صِدۡقٖ وَأَخۡرِجۡنِي مُخۡرَجَ صِدۡقٖ وَٱجۡعَل لِّي مِن لَّدُنكَ سُلۡطَٰنٗا نَّصِيرٗا

Na useme, «Mola wangu! Nitia matio mazuri katika jambo lililo lema kwangu na unitoe matoko mazuri kwenye mambo yaliyo mabaya kwangu, na unipatie hoja thabiti kutoka kwako yenye kuniokoa na wote wanaoenda kinyume na mimi.» info
التفاسير:

external-link copy
81 : 17

وَقُلۡ جَآءَ ٱلۡحَقُّ وَزَهَقَ ٱلۡبَٰطِلُۚ إِنَّ ٱلۡبَٰطِلَ كَانَ زَهُوقٗا

Na useme, ewe Mtume, kuwaambia washirikina, «Uislamu umekuja na ushirikina umeondoka. Kwani ubatilifu hauna kusalia wala kujikita, na ukweli ndio wenye kuimarika na kusalia ambao hauondoki.» info
التفاسير:

external-link copy
82 : 17

وَنُنَزِّلُ مِنَ ٱلۡقُرۡءَانِ مَا هُوَ شِفَآءٞ وَرَحۡمَةٞ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ وَلَا يَزِيدُ ٱلظَّٰلِمِينَ إِلَّا خَسَارٗا

Na tunateremsha miongoni mwa aya za Qur’ani yanayopoza magonjwa ya nyoyo kama shaka , unafiki na ujinga, na yanayopoza miili kwa kujizungua nayo, na yanayokuza Imani ambayo ni sababu ya kufaulu kupata rehema ya Mwenyezi Mungu. Na hii Qur’ani haiwaongezei makafiri wanapoisikia isipokua ukafiri na upotevu, kwa kuikanusha kwao na kutoiamini. info
التفاسير:

external-link copy
83 : 17

وَإِذَآ أَنۡعَمۡنَا عَلَى ٱلۡإِنسَٰنِ أَعۡرَضَ وَنَـَٔا بِجَانِبِهِۦ وَإِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ كَانَ يَـُٔوسٗا

Na tunapompa mwanadamu, vile alivyo, neema ya mali na afya na mfano wa hizo, anageuka na kujiweka mbali na kumtii Mwenyezi Mungu, na akipatikana na shida ya ufukara au ugonjwa huwa ni mwenye kukata tamaa, kwa kuwa yeye haamini kuwa atapata nyongeza njema za Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, isipokuwa yule ambaye Mwenyezi Mungu Amemuhifadhi katika hali yake ya raha na ya shida. info
التفاسير:

external-link copy
84 : 17

قُلۡ كُلّٞ يَعۡمَلُ عَلَىٰ شَاكِلَتِهِۦ فَرَبُّكُمۡ أَعۡلَمُ بِمَنۡ هُوَ أَهۡدَىٰ سَبِيلٗا

Sema, ewe Mtume, kuwaambia watu, «Kila mmoja miongoni mwenu anatenda kulingana na hali zinazonasibiana na yeye , na Mola wenu ni Mjuzi zaidi wa yule aliyeongoka zaidi njia ya haki.» info
التفاسير:

external-link copy
85 : 17

وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلرُّوحِۖ قُلِ ٱلرُّوحُ مِنۡ أَمۡرِ رَبِّي وَمَآ أُوتِيتُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِ إِلَّا قَلِيلٗا

Na makafiri wanakuuliza juu ya uhakika wa roho kwa njia ya ushindani, basi wajibu kwamba uhakika wa roho na hali zake ni katika mambo ambayo Mwenyezi Mungu Ameufanya ujuzi wake uweko Kwake. Na hamukupewa ujuzi, nyinyi na watu wote, isipokuwa kitu kichache. info
التفاسير:

external-link copy
86 : 17

وَلَئِن شِئۡنَا لَنَذۡهَبَنَّ بِٱلَّذِيٓ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ ثُمَّ لَا تَجِدُ لَكَ بِهِۦ عَلَيۡنَا وَكِيلًا

Na lau tulitaka kuifuta Qur’ani moyoni mwake, tungaliliweza hilo, na hungalimpata mwenye kukuhami ambaye atatuzuia kufanya hivyo au akurudishie Qur’ani. info
التفاسير: