クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis

ページ番号:close

external-link copy
35 : 13

۞ مَّثَلُ ٱلۡجَنَّةِ ٱلَّتِي وُعِدَ ٱلۡمُتَّقُونَۖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۖ أُكُلُهَا دَآئِمٞ وَظِلُّهَاۚ تِلۡكَ عُقۡبَى ٱلَّذِينَ ٱتَّقَواْۚ وَّعُقۡبَى ٱلۡكَٰفِرِينَ ٱلنَّارُ

Sifa ya Pepo ambayo Mwenyezi Mungu Amewaahidi nayo wale wanaomuogopa na kwamba mito inapita chini ya miti yake na majumba yake ya fahari, Matunda yake hayamaliziki na kivuli chake hakiondoki. Malipo mema hayo ya Pepo ndio mwisho wa waliomuogopa Mwenyezi Mungu wakajiepusha na mambo ya kumuasi na wakatekeleza faradhi Zake. Na mwisho wa makafiri ni Moto. info
التفاسير:

external-link copy
36 : 13

وَٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يَفۡرَحُونَ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَۖ وَمِنَ ٱلۡأَحۡزَابِ مَن يُنكِرُ بَعۡضَهُۥۚ قُلۡ إِنَّمَآ أُمِرۡتُ أَنۡ أَعۡبُدَ ٱللَّهَ وَلَآ أُشۡرِكَ بِهِۦٓۚ إِلَيۡهِ أَدۡعُواْ وَإِلَيۡهِ مَـَٔابِ

Na wale ambao tuliwapa Kitabu, miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara, yoyote kati yao mwenye kukuamini, kama 'Abdullāh bin Salām na Najashi, wanaifurahia Qur’ani uliyoteremshiwa kwa kuwa inaenda sambamba na kile walichonacho. Na miongoni mwa wale wanaojiweka pamoja kukupinga, kama Sayyid na 'Aqib: maaskofu wawili wa Najran , na Ka'b bin al-Ashraf, wanaokanusha baadhi ya yale uliyoteremshiwa. Waambie, «Mwenyezi Mungu Ameniamrisha nimuabudu Yeye Peke Yake na nisimshirikishe chochote. Nawaita watu wamuabudu, na Kwake Peke Yake ndio marejeo yangu na marudio. info
التفاسير:

external-link copy
37 : 13

وَكَذَٰلِكَ أَنزَلۡنَٰهُ حُكۡمًا عَرَبِيّٗاۚ وَلَئِنِ ٱتَّبَعۡتَ أَهۡوَآءَهُم بَعۡدَ مَا جَآءَكَ مِنَ ٱلۡعِلۡمِ مَا لَكَ مِنَ ٱللَّهِ مِن وَلِيّٖ وَلَا وَاقٖ

Na kama tulivyowateremshia Mitume Vitabu kwa lugha zao, tulikuteremshia wewe, ewe Mtume, Qur’ani kwa lugha ya Kiarabu, ili uitumie katika kuhukumu. Na lau ulifuata mapendeleo ya washirikina katika kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu, baada ya haki iliyokujia kutoka kwa Mwenyezi Mungu, hutakuwa na msaidizi yoyote mwenye kukuhami na kuzuia adhabu ya Mwenyezi Mungu isikufikie. info
التفاسير:

external-link copy
38 : 13

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا رُسُلٗا مِّن قَبۡلِكَ وَجَعَلۡنَا لَهُمۡ أَزۡوَٰجٗا وَذُرِّيَّةٗۚ وَمَا كَانَ لِرَسُولٍ أَن يَأۡتِيَ بِـَٔايَةٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۗ لِكُلِّ أَجَلٖ كِتَابٞ

Na kumbuka waliposema, «Una nini, ewe Mtume, unaoa wanawake?» Hakika tulituma kabla yako Mitume kati ya wanadamu na kuwafanya wawe na wake na watoto. Na pia utaje waliposema, «Lau alikuwa ni Mtume angalituletea miujiza tuliyoitaka.» Haiko kwenye uwezo wa Mtume yoyote, kuleta miujiza ambayo watu wake waliitaka isipokuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Kila jambo alilolihukumu Mwenyezi Mungu lina maandishi na wakati, Mwenyezi Mungu Ameliandika hapo Kwake, halitangulii wala halichelewi. info
التفاسير:

external-link copy
39 : 13

يَمۡحُواْ ٱللَّهُ مَا يَشَآءُ وَيُثۡبِتُۖ وَعِندَهُۥٓ أُمُّ ٱلۡكِتَٰبِ

Mwenyezi Mungu Anakifuta Akitakacho miongoni mwa hukumu na mengineyo, na Anakiacha kisalie Akitakacho miongoni mwa hizo kwa hekima fulani Anayoijua. Na Kwake kuna asili ya Kitabu, nacho ni Al-Lawh„ Al-Mah,fūd,: Ubao uliohifadhiwa ambao yamethibitishwa ndani yake kimaandishi hali za viumbe mpaka Siku ya Kiyama. info
التفاسير:

external-link copy
40 : 13

وَإِن مَّا نُرِيَنَّكَ بَعۡضَ ٱلَّذِي نَعِدُهُمۡ أَوۡ نَتَوَفَّيَنَّكَ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُ وَعَلَيۡنَا ٱلۡحِسَابُ

Na tukikuonesha , ewe Mtume, baadhi ya mateso tuliyowaahidi maadui zako ya kuhizika na kuungulika ulimwenguni, basi hayo ni yale tuliyowaharakishia. Na tukikufisha kabla hujaona hayo, basi wajibu wako haukuwa isipokuwa ni kutekeleza ulinganizi, na hesabu na malipo ni juu yetu. info
التفاسير:

external-link copy
41 : 13

أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّا نَأۡتِي ٱلۡأَرۡضَ نَنقُصُهَا مِنۡ أَطۡرَافِهَاۚ وَٱللَّهُ يَحۡكُمُ لَا مُعَقِّبَ لِحُكۡمِهِۦۚ وَهُوَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Kwani hawaoni hawa makafiri kwamba sisi tunaijia ardhi na kuipunguza pambizoni mwake kwa kuwapa Waislamu ushindi wa kuiteka miji ya makafiri na kuishikanisha na miji ya Kiislamu? Na Mwenyezi Mungu Anaamua, hakuna Mwenye kuurudi uamuzi Wake na hukumu Yake. Na Yeye ni Mpesi wa kuhesabu, basi wasifanye haraka ya kutaka kuletewa adhabu, kwani kila lenye kuja liko karibu. info
التفاسير:

external-link copy
42 : 13

وَقَدۡ مَكَرَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ فَلِلَّهِ ٱلۡمَكۡرُ جَمِيعٗاۖ يَعۡلَمُ مَا تَكۡسِبُ كُلُّ نَفۡسٖۗ وَسَيَعۡلَمُ ٱلۡكُفَّٰرُ لِمَنۡ عُقۡبَى ٱلدَّارِ

Hakika wale waliokuwa kabla yao waliwapangia njama Mitume wao, kama vile hawa walivyokufanyia. Basi vitimbi vyote vina Mwenyezi Mungu, Anatangua vitimbi vyao na kuwarudishia wenyewe wapite patupu na wajute. Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu Kwake, Anakijua kile ambacho kila mtu anakichuma, chema au kibaya, na atalipwa kwa hicho. Na watajuwa makafiri, watakapofika kwa Mola wao, ni nanani atakuwa na mwisho mwema baada ya dunia hii. Huo ni wa wafuasi wa Mitume. Katika haya kuna onyo na tishio kwa makafiri. info
التفاسير: