क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अली मुहसिन बरवानी

पृष्ठ संख्या:close

external-link copy
38 : 3

هُنَالِكَ دَعَا زَكَرِيَّا رَبَّهُۥۖ قَالَ رَبِّ هَبۡ لِي مِن لَّدُنكَ ذُرِّيَّةٗ طَيِّبَةًۖ إِنَّكَ سَمِيعُ ٱلدُّعَآءِ

Pale pale Zakariya akamwomba Mola wake Mlezi, akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe kutoka kwako uzao mwema. Wewe ndiye unaye sikia maombi. info

Zakariya a.s. alipo iona neema ya Mwenyezi Mungu kwa Maryamu alimwelekea Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu akimwomba kwa fadhila yake na ukarimu wake na uwezo wake, naye ampe mtoto mwanamume. Kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia maombi ya mwenye kuomba kwake kwa unyenyekevu. Naye ni Muweza wa kuitikia maombi na hata zinge kuwapo pingamizi za kikawaida kama ukongwe na utasa.

التفاسير:

external-link copy
39 : 3

فَنَادَتۡهُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ وَهُوَ قَآئِمٞ يُصَلِّي فِي ٱلۡمِحۡرَابِ أَنَّ ٱللَّهَ يُبَشِّرُكَ بِيَحۡيَىٰ مُصَدِّقَۢا بِكَلِمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَسَيِّدٗا وَحَصُورٗا وَنَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Alipo kuwa kasimama chumbani akiswali, Malaika kamnadia: Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria Yahya, ataye kuwa mwenye kusadikisha neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu, na ni bwana na mt'awa na Nabii kwa watu wema. info

Mwenyezi Mungu aliitikia dua yake. Malaika akamnadia naye kasimama pahala pake pa ibada akimwelekea Mola wake Mlezi kumbashiria mtoto mwanamume jina lake Yahya, atakaye muamini Isa a.s. ambaye atazaliwa kwa kauli ya Mwenyezi Mungu kwa njia isiyo ya dasturi. Na Yahya atawahimiza kaumu yake kushika ilimu na kuswali, na atakataza mambo ya pumbao na matamanio, na atamfanya awe miongoni mwa Manabii na watu wema.

التفاسير:

external-link copy
40 : 3

قَالَ رَبِّ أَنَّىٰ يَكُونُ لِي غُلَٰمٞ وَقَدۡ بَلَغَنِيَ ٱلۡكِبَرُ وَٱمۡرَأَتِي عَاقِرٞۖ قَالَ كَذَٰلِكَ ٱللَّهُ يَفۡعَلُ مَا يَشَآءُ

Akasema Zakariya: Mola wangu Mlezi! Vipi nitapata mwana na hali ukongwe umenifikia, na mke wangu ni tasa? Akasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu hufanya apendavyo. info

Basi Zakariya alipo pewa bishara hii, ya kupata mwana, alimwelekea Mola Mlezi wake kwa shauku ya kutaka kujua vipi yatakuwa hayo, ya kuwa na mwana na ilhali yeye hanazo njia zijuulikanazo, kwa kuwa yeye mwenyewe kesha konga, na mkewe ni tasa. Mwenyezi Mungu akamjibu kuwa Yeye anapo taka jambo ama huzileta njia au huumba bila ya njia zinazo juulikana. Kwani Yeye hutenda apendavyo.

التفاسير:

external-link copy
41 : 3

قَالَ رَبِّ ٱجۡعَل لِّيٓ ءَايَةٗۖ قَالَ ءَايَتُكَ أَلَّا تُكَلِّمَ ٱلنَّاسَ ثَلَٰثَةَ أَيَّامٍ إِلَّا رَمۡزٗاۗ وَٱذۡكُر رَّبَّكَ كَثِيرٗا وَسَبِّحۡ بِٱلۡعَشِيِّ وَٱلۡإِبۡكَٰرِ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Niwekee alama. Akasema: Alama yako ni kuwa hutasema na watu kwa siku tatu, isipo kuwa kwa kuashiria tu. Na mdhukuru Mola Mlezi wako kwa wingi na mtakase jioni na asubuhi. info

Zakariya akamwomba Mola wake Mlezi amfanyie alama ya kuhakikisha bishara hii. Mwenyezi Mungu akamjibu: Alama yako ni kuwa hutaweza kusema na watu muda wa siku tatu, isipo kuwa utatumia ishara tu kuashiria utakacho. Na shikamana na dhikri ya Mwenyezi Mungu ukimtakasa na kumtukuza jioni na asubuhi.

التفاسير:

external-link copy
42 : 3

وَإِذۡ قَالَتِ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ يَٰمَرۡيَمُ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰكِ وَطَهَّرَكِ وَٱصۡطَفَىٰكِ عَلَىٰ نِسَآءِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na angalia pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Kwa hakika Mwenyezi Mungu amekuteuwa, na akakutakasa, na akakutukuza kuliko wanawake wote. info

Na kumbuka ewe Nabii, pale Malaika walipo mwambia Maryamu ya kwamba Mwenyezi Mungu amekukhitari uwe ni mama wa Nabii wake, na amekusafisha na kila uchafu, na amekuteuwa wewe uwe mama wa Isa kuliko wanawake wote wengineo.

التفاسير:

external-link copy
43 : 3

يَٰمَرۡيَمُ ٱقۡنُتِي لِرَبِّكِ وَٱسۡجُدِي وَٱرۡكَعِي مَعَ ٱلرَّٰكِعِينَ

Ewe Maryamu! Mnyenyekee Mola Mlezi wako na usujudu na uiname pamoja na wainamao. info

Na kwa haya ewe Maryamu, yanakuwajibikia wewe umshukuru Mola wako Mlezi. Basi jilazimishe ut'iifu kwake, na uwe mwenye kushika Swala, na shirikiana na wengine wanao muabudu Mwenyezi Mungu na wanaswali kwa ajili yake.

التفاسير:

external-link copy
44 : 3

ذَٰلِكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلۡغَيۡبِ نُوحِيهِ إِلَيۡكَۚ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ يُلۡقُونَ أَقۡلَٰمَهُمۡ أَيُّهُمۡ يَكۡفُلُ مَرۡيَمَ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ

Hizi ni khabari za ghaibu tunazo kufunulia; nawe hukuwa nao walipo kuwa wakitupa kalamu zao nani wao atamlea Maryamu, na hukuwa nao walipo kuwa wakishindana. info

Haya unayo simuliwa wewe Muhammad na Qur'ani ni katika khabari tukufu za wale alio wateuwa Mwenyezi Mungu, nazo ni khabari za ghaibu ambazo Mwenyezi Mungu anakufunulia. Na wala wewe hukuwapo wakati walipo kuwa wakipiga kura kwa mishale, ili waweze kukata shauri juu ya Maryamu. Na wala wewe hukuwapo walipo gombana kuwania nani wa kupata cheo hicho kitukufu.

التفاسير:

external-link copy
45 : 3

إِذۡ قَالَتِ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ يَٰمَرۡيَمُ إِنَّ ٱللَّهَ يُبَشِّرُكِ بِكَلِمَةٖ مِّنۡهُ ٱسۡمُهُ ٱلۡمَسِيحُ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ وَجِيهٗا فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu). info

Kumbuka na utaje ewe Nabii, pale Malaika walipo mbashiria Maryamu kuwa atamzaa mwana kwa neno lake tu Mwenyezi Mungu kinyume na ada wanavyo zaliwa watu. Jina lake mwana huyo ni Masihi Isa bin Maryamu. Na Mwenyezi Mungu amemjaalia hapa duniani kuwa atakuwa na cheo kwa unabii wake na kuepukana na aibu zote, na kesho Akhera kuwa atakuwa na cheo cha juu pamoja na kundi la walio takasika, wakawa wenye kuwa karibu mno na Mwenyezi Mungu miongoni mwa Manabii walio imara baraabara.

التفاسير: