Na siku atakapo waita na akasema: Wako wapi hao mlio kuwa mkidai kuwa ni washirika wangu?
Na pia, ewe Mtume, kumbuka siku watapo itwa washirikina na Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa wito wa kuwatahayarisha, wakaambiwa: Wako wapi washirika ambao mkidai kuwa ni miungu wa kukunusuruni, au waombezi wa kukuombeeni?