Traduction des sens du Noble Coran - La traduction swahili - 'Abd Allah Muhammad et Nâsir Khamîs

Adh-Dhariyat

external-link copy
1 : 51

وَٱلذَّٰرِيَٰتِ ذَرۡوٗا

Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anaapa kwa upepo wenye kurusha mchanga, info
التفاسير:

external-link copy
2 : 51

فَٱلۡحَٰمِلَٰتِ وِقۡرٗا

na mawingu yenye kubeba uzito mkubwa wa maji, info
التفاسير:

external-link copy
3 : 51

فَٱلۡجَٰرِيَٰتِ يُسۡرٗا

na jahazi zinazopita baharini na kutembea kwa upesi na usahali, info
التفاسير:

external-link copy
4 : 51

فَٱلۡمُقَسِّمَٰتِ أَمۡرًا

na Malaika wenye kugawanya amri za Mwenyezi Mungu kwa viumbe Vyake, info
التفاسير:

external-link copy
5 : 51

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٞ

kwamba mnayoahidiwa, enyi watu, ya kufufuliwa na kuhesabiwa ni tukio lenye kuwa kwa kweli na yakini, info
التفاسير:

external-link copy
6 : 51

وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٞ

na kwamba kuhesabiwa na kulipwa mema kwa amali njema ni jambo lisilo na budi. info
التفاسير: