[1] Wanaitakidi kwa ujinga wao kuwa wao wanamhadaa Mwenyezi Mungu na Waumini kwa kudhihirisha kwao Imani na kuficha kwao ukafiri. Nao hawamhadai yoyote isipokuwa wao wenyewe, kwa kuwa, madhara ya kuhadaa kwao yanawarudia wao. Na kwa sababu ujinga wao umekolea na nyoyo zao zimeharibika, huwa hawana hisia ya hilo. (Tafsir Muyasar cha jopo la wanachuoni)