[1] Kwa sababu Qur-ani ndio uwongofu wao, limetumika neno "juu" ili kuifananisha hali ya kuimarika kwa Waumini katika uwongofu na uthabiti wao juu yake; na kujaribu kwao kuuongeza na kutembea katika njia za heri. Na mwonekano wa (mtu) aliyepanda kipando (kama farasi) katika kuwa kwake juu ya kipando hicho, na uwezo wake wa kukiendesha na kukifanya kuwa kitiifu. (Tafsir At-Tahrir Wat-tanwiir cha Ibn 'Aashuur)