Enyi Waumini! Msiwafanye baba zenu, na watoto wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na wake zenu, ndio wasaidizi wenu wa kukunusuruni maadamu wanapenda ukafiri, na wanaufadhilisha kuliko Imani. Na wenye kutaka manusura kwa makafiri, ndio hao walio iwacha Njia Iliyo Nyooka.