Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis

external-link copy
21 : 8

وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ قَالُواْ سَمِعۡنَا وَهُمۡ لَا يَسۡمَعُونَ

Wala msiwe, enyi Waumini, katika kwenda kinyume kwenu na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, rehema na amani zimshukiye, ni kama washirikina na wanafiki ambao wakisikia Kitabu cha Mwenyezi Mungu kinasomwa kwao huwa wakisema, «Tumesikia kwa masikio yetu,» na hali wao kwa hakika hawayazingatii wanayoyasikia wala hawayatii akilini. info
التفاسير: