Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis

external-link copy
200 : 7

وَإِمَّا يَنزَغَنَّكَ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ نَزۡغٞ فَٱسۡتَعِذۡ بِٱللَّهِۚ إِنَّهُۥ سَمِيعٌ عَلِيمٌ

Na iwapo utashikwa na hasira, ewe Nabii, zitokazo kwa Shetani au ukahisi, kutoka kwake, wasiwasi au ulegevu wa kufanya mema au himizo la kufanya ovu, basi tafuta himaya kwa Mola wako kwa kujilinda Kwake. Kwani Yeye ni Msikizi wa kila neno ni Mjuzi wa kila kitendo. info
التفاسير: