Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis

At-Tur

external-link copy
1 : 52

وَٱلطُّورِ

Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Ṭūr, nalo ni jabali ambalo juu yake Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Alizungumza na Mūsā. info
التفاسير:

external-link copy
2 : 52

وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na kwa Kitabu kilichoandikwa, nacho ni Qur’ani, info
التفاسير:

external-link copy
3 : 52

فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

kwenye nyaraka zilizokunjuliwa. info
التفاسير:

external-link copy
4 : 52

وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na kwa Nyumba Iliyoamirishwa kwa Malaika watukufu wenye kuizunguka daima. info
التفاسير:

external-link copy
5 : 52

وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na kwa sakafu iliyoinuliwa juu, nayo ni uwingu wa duniani. info
التفاسير:

external-link copy
6 : 52

وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na kwa bahari iliyowashwa moto, iliyojaa maji. info
التفاسير:

external-link copy
7 : 52

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

Hakika adhabu ya Mola Wako, ewe Mtume, ni yenye kuwashukia makafiri. info
التفاسير:

external-link copy
8 : 52

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hakuna kizuizi cha kuizuia itakaposhuka. info
التفاسير:

external-link copy
9 : 52

يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku ya mbingu kutetemeka mpango wake kuharibika na pande zake kusukikasukika, na hapo ni wakati wa mwisho wa dunia, info
التفاسير:

external-link copy
10 : 52

وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

na majabali yaondoke mahali pake na yatembee kama vile mawingu yanavyotembea. info
التفاسير:

external-link copy
11 : 52

فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Maangamivu katika Siku hii ni yenye kuwashukia wakanushaji. info
التفاسير:

external-link copy
12 : 52

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ

Ambao wao wamevama ndani ya ubatilifu wanapumbaa nao na wanaifanya dini yao kuwa ni shere na mchezo. info
التفاسير:

external-link copy
13 : 52

يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Siku ya kusukumwa hawa wakanushaji msukumo wa nguvu wenye kuwadhalilisha hadi kwenye Moto wa Jahanamu. info
التفاسير:

external-link copy
14 : 52

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Na waambiwe kwa njia ya kuwalaumu na kuwakaripia, «Huu ndio huo Moto ambao mlikuwa mkiukanusha! info
التفاسير: