Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis

external-link copy
31 : 47

وَلَنَبۡلُوَنَّكُمۡ حَتَّىٰ نَعۡلَمَ ٱلۡمُجَٰهِدِينَ مِنكُمۡ وَٱلصَّٰبِرِينَ وَنَبۡلُوَاْ أَخۡبَارَكُمۡ

Na tutawatahini nyinyi, tena tutawatahini, enyi Waumini, kwa kupambana na maadui wa Mwenyezi Mungu na kupigana nao jihadi mpaka yajitokeze yale Aliyoyajua Mwenyezi Mungu tangu kale, ili tuwatenge watu wa jihadi kati yenu na uvumilivu wa kupigana na maadui wa Mwenyezi Mungu na tuyatahini maneno yenu na matendo yenu, na hapo adhihirike mkweli miongoni mwenu kutokana na mrongo. info
التفاسير: