Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdullah Muhammad & Naser Khamis

external-link copy
29 : 3

قُلۡ إِن تُخۡفُواْ مَا فِي صُدُورِكُمۡ أَوۡ تُبۡدُوهُ يَعۡلَمۡهُ ٱللَّهُۗ وَيَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Sema, ewe Nabii, Kuwaambia Waumini, «Mkiyaficha yaliyomo ndani ya nyoyo zenu ya kuwafanya makafiri ni wategemewa na wasaidizi au mkiyadhihirisha hayo, hakitafichika chochote katika hayo kwa Mwenyezi Mungu. Kwani ujuzi Wake umezunguka kila kilichoko mbinguni na kilichoko ardhini, na Ana uwezo kamili juu ya kila kitu. info
التفاسير: