Prijevod značenja časnog Kur'ana - Prijevod na svahili jezik - Abdullah Muhammed i Nasir Hamis

Broj stranice:close

external-link copy
23 : 33

مِّنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ رِجَالٞ صَدَقُواْ مَا عَٰهَدُواْ ٱللَّهَ عَلَيۡهِۖ فَمِنۡهُم مَّن قَضَىٰ نَحۡبَهُۥ وَمِنۡهُم مَّن يَنتَظِرُۖ وَمَا بَدَّلُواْ تَبۡدِيلٗا

Miongoni mwa Waumini kuna wanaume waliotekeleza ahadi zao walizomuahidi Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na wakasubiri juu ya shida, madhara na wakati wa vita. Kati yao kuna aliyetekeleza nadhiri akafa shahidi katika njia ya Mwenyezi Mungu au akafa juu ya ukweli na utekelezaji ahadi, na kati yao kuna anayengojea mojawapo ya mema mawili, ushindi au kufa shahidi, na hawakuigeuza ahadi ya Mwenyezi Mungu wala hawakuitangua wala hawakuibadilisha kama vile wanafiki walivyogeuza. info
التفاسير:

external-link copy
24 : 33

لِّيَجۡزِيَ ٱللَّهُ ٱلصَّٰدِقِينَ بِصِدۡقِهِمۡ وَيُعَذِّبَ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ إِن شَآءَ أَوۡ يَتُوبَ عَلَيۡهِمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Ili Mwenyezi Mungu Awalipe mema watu wa ukweli kwa ukweli wao na kujitolea kwao, nao ni Waumini, na ili Awaadhibu wanafiki Akitaka kuwaadhibu, kwa kutowapa taufiki ya kutubia toba ya kidhati kabla ya kufa, hivyo basi wafe kwenye ukafiri na wastahili Moto, au Awape taufiki ya kutubia na kurejea, kwani Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe dhambi za wenye kuzidhulumu nafsi zao, ni Mwingi wa huruma kwao kwa kuwapa taufiki ya kutubia toba ya kidhati. info
التفاسير:

external-link copy
25 : 33

وَرَدَّ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِغَيۡظِهِمۡ لَمۡ يَنَالُواْ خَيۡرٗاۚ وَكَفَى ٱللَّهُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ ٱلۡقِتَالَۚ وَكَانَ ٱللَّهُ قَوِيًّا عَزِيزٗا

Na Akayarudisha Mwenyezi Mungu mapote ya ukafiri kutoka Madina yakiwa yamepita patupu, yamepata hasara na yamejawa na hasira, hayakupata kheri yoyote duniani wala Akhera, na Mwenyezi Mungu Akawatosheleza Waumini (wasilazimike) kupigana kwa kuwasaidia kwa sababu Alizowatolea. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Hashindwi wala Halazimishwi, ni Mshindi katika ufalme Wake na mamlaka Yake. info
التفاسير:

external-link copy
26 : 33

وَأَنزَلَ ٱلَّذِينَ ظَٰهَرُوهُم مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ مِن صَيَاصِيهِمۡ وَقَذَفَ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلرُّعۡبَ فَرِيقٗا تَقۡتُلُونَ وَتَأۡسِرُونَ فَرِيقٗا

Na Mwenyezi Mungu Akawateremsha Mayahudi wa Banū Qurayẓah kutoka kwenye ngome zao kwa kuwa waliyasaidia Mapote katika kupigana na Waislamu, na Akatia hofu ndani ya nyoyo zao wakashindwa, mkawa mnaua kundi katika wao na mnateka kundi lingine. info
التفاسير:

external-link copy
27 : 33

وَأَوۡرَثَكُمۡ أَرۡضَهُمۡ وَدِيَٰرَهُمۡ وَأَمۡوَٰلَهُمۡ وَأَرۡضٗا لَّمۡ تَطَـُٔوهَاۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٗا

Na Akawamilikisha nyinyi, enyi Waumini, ardhi yao, makazi yao na mali yao yanayohamishika kama vile pambo, silaha na wanyama na yasiyohamishika kama vile mashamba, nyumba na ngome zilizojikita. Na Akawarithisha ardhi ambayo hamkuweza kuikanyaga kabla ya hapo. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu, hakuna kinachomshinda. info
التفاسير:

external-link copy
28 : 33

يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ قُل لِّأَزۡوَٰجِكَ إِن كُنتُنَّ تُرِدۡنَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا وَزِينَتَهَا فَتَعَالَيۡنَ أُمَتِّعۡكُنَّ وَأُسَرِّحۡكُنَّ سَرَاحٗا جَمِيلٗا

Ewe Nabii! Waambie wake zako waliojikusanya mbele yako wakitaka kwako ongezo la matumizi, «Mkiwa mnataka maisha ya kilimwengu na pambo lake, basi njooni niwastareheshe kwa kitu kichache cha kilimwengu nilicho nacho na niwatenge bila ya kuwadhuru wala kuwaudhi. info
التفاسير:

external-link copy
29 : 33

وَإِن كُنتُنَّ تُرِدۡنَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَٱلدَّارَ ٱلۡأٓخِرَةَ فَإِنَّ ٱللَّهَ أَعَدَّ لِلۡمُحۡسِنَٰتِ مِنكُنَّ أَجۡرًا عَظِيمٗا

«Na mkiwa mnataka radhi ya Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na yale aliyowaandalia Mwenyezi Mungu katika Nyumba ya Akhera, basi vumilieni juu ya hali mliyonayo, na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, kwani hakika Mwenyezi Mungu Amewaandalia walio wema katika nyinyi malipo makubwa.» (Na walimchagua Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na yale Aliyowaandalia Mwenyezi Mungu katika Nyumba ya Akhera). info
التفاسير:

external-link copy
30 : 33

يَٰنِسَآءَ ٱلنَّبِيِّ مَن يَأۡتِ مِنكُنَّ بِفَٰحِشَةٖ مُّبَيِّنَةٖ يُضَٰعَفۡ لَهَا ٱلۡعَذَابُ ضِعۡفَيۡنِۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ يَسِيرٗا

Enyi wake za Mtume! Yoyote miongoni mwenu Atakayefanya maasia yaliyo wazi ataongezewa adhabu mara mbili zaidi.( Na kwa kuwa cheo chao ni cha juu, imenasibiana na cheo hicho Mwenyezi Mungu Alifanye dhambi linalotokana na wao liwe zito, ili kuhifadhi heshima yao na heshima ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, Na kuadhibu huko ni rahisi kwa Mwenyezi Mungu. info
التفاسير: