আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- আলী মুহছিন আল-বাৰওৱানী

Al-Mursalat

external-link copy
1 : 77

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا

Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!  info

Naapa kwa Aya zilizo tumwa kwa ulimi wa Jibrili kumpelekea Muhammad kwa upole wa kawaida na kheri,

التفاسير:

external-link copy
2 : 77

فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا

Na zinazo vuma kwa kasi! info

Na kwa Aya zenye kuzitwaa kwa nguvu dini nyengine zote za uwongo zikizipeperushia mbali,

التفاسير:

external-link copy
3 : 77

وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا

Na zikaeneza maeneo yote! info

Na kwa Aya zenye kueneza hikima na uwongofu katika nyoyo za walimwengu kwa uenezi mkubwa mno,

التفاسير:

external-link copy
4 : 77

فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا

Na zinazo farikisha zikatawanya! info

Na zenye kufarikisha baina ya kweli na uwongo kwa mfarakano ulio wazi kabisa,

التفاسير:

external-link copy
5 : 77

فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا

Na zinazo peleka mawaidha! info

Na zenye kuwapa watu mawaidha ya kuwanufaisha,

التفاسير:

external-link copy
6 : 77

عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا

Kwa kuudhuru au kuonya, info

Ili iwe ni udhuru kwao na onyo wasiwe na hoja,

التفاسير:

external-link copy
7 : 77

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa! info

Hakika haya mliyo ahidiwa ya kuja Kiyama kwa yakini yatatimia tu bila ya shaka yoyote.

التفاسير:

external-link copy
8 : 77

فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ

Wakati nyota zitakapo futwa, info

Basi nyota zitapo ondolewa kabisa,

التفاسير:

external-link copy
9 : 77

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ

Na mbingu zitakapo pasuliwa, info

Na mbingu zitapo pasuka,

التفاسير:

external-link copy
10 : 77

وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ

Na milima itakapo peperushwa, info

Na milima ikavurugwa na ikapeperushiwa mbali na upepo,

التفاسير:

external-link copy
11 : 77

وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ

Na Mitume watakapo wekewa wakati wao, info

Na Mitume wakawekewa wakati maalumu wahudhurie kwa ajili ya kuwatolea ushahidi kaumu zao.

التفاسير:

external-link copy
12 : 77

لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo? info

Kwa ajili ya siku gani yametayarishwa mambo haya makubwa makubwa?

التفاسير:

external-link copy
13 : 77

لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ

Kwa siku ya kupambanua! info

Kwa ajili ya siku watakapo pambanuliwa baina ya viumbe.

التفاسير:

external-link copy
14 : 77

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ

Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini? info

Na nini cha kukujuvya ina nini hiyo siku ya kupambanua?

التفاسير:

external-link copy
15 : 77

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha! info

Ni maangamio ya milele siku hiyo kwa hao wanao kadhibisha walio waahidi Mitume!

التفاسير:

external-link copy
16 : 77

أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia? info

Kwani hatukuwaangamiza mataifa ya zamani yaliyo kadhibisha,

التفاسير:

external-link copy
17 : 77

ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ

Kisha tukawafuatilizia walio fuatia? info

Na kisha tukawafuatilizia hao wenginewe tukawateketeza hali kadhaalika,

التفاسير:

external-link copy
18 : 77

كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu! info

Kwa madhambi waliyo yafanya na walivyo mkataa Mwenyezi Mungu?

التفاسير:

external-link copy
19 : 77

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha! info

Siku hiyo ni siku ya kuteketezwa walio kadhibisha, kama tulivyo waahidi.

التفاسير: