ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

سورة النازعات - An-Nazi'at

external-link copy
1 : 79

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا

Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu! info

Ninaapa kwa kila kilicho pewa uwezo wa kuving'oa vitu kutokana na pahala pao kwa nguvu,

التفاسير:

external-link copy
2 : 79

وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا

Na kwa wanao toa kwa upole! info

Na kwa kila kilicho pewa uwezo wa kuvitoa vitu kwa utaratibu na ulaini,

التفاسير:

external-link copy
3 : 79

وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا

Na wanao ogelea! info

Na kwa kila kilicho pewa mbio za kutekeleza kazi yake kwa sahala na wepesi.

التفاسير:

external-link copy
4 : 79

فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا

Wakishindana mbio! info

Na kwa vinavyo shindania kutimiza waajibu ulio twikwa juu yao kushindania kwa juhudi,

التفاسير:

external-link copy
5 : 79

فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا

Wakidabiri mambo. info

Na vinavyo dabiri, kupanga, mambo na kuyaendesha kwa mujibu wa vilivyo khusishwa,

التفاسير:

external-link copy
6 : 79

يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ

Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka! info

Bila ya shaka Saa ya Kiyama itafika; hiyo siku ambayo mpulizo wa mwanzo wa barugumu utavitikisa viumbe vyote,

التفاسير:

external-link copy
7 : 79

تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ

Kifuate cha kufuatia. info

Na mpulizo huo utafuatiwa na wa pili ambao ndio utakao kuwa wa kufufuliwa watu.

التفاسير:

external-link copy
8 : 79

قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ

Siku hiyo nyoyo zitapiga piga! info

Siku hiyo nyoyo zitapapatika kwa khofu.

التفاسير:

external-link copy
9 : 79

أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ

Macho yatainama chini! info

Macho ya watu yatakuwa na huzuni, manyonge.

التفاسير:

external-link copy
10 : 79

يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ

Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza? info

Watu hawa husema duniani kwa kukanya kufufuliwa: Ati tutarudishwa sisi baada ya kwisha kufa, tuumbwe tena kama tulivyo kuwa?

التفاسير:

external-link copy
11 : 79

أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ

Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa? info

Tukisha kuwa mafupa yaliyo chakaa, ati tutarejeshwa tufufuliwe upya?

التفاسير:

external-link copy
12 : 79

قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ

Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara! info

Wanasema, kwa kukanya na kejeli: Kurejea huko kama kukitokea basi ni marejeo ya khasara, na sisi si watu wa kukhasiri.

التفاسير:

external-link copy
13 : 79

فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu, info

Msidhani kurejea huko ni kuzito. Kwani hayo ni ukelele mmoja tu,

التفاسير:

external-link copy
14 : 79

فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ

Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano! info

Mara maiti wote watahudhurishwa kwenye ardhi ya mkusanyiko!

التفاسير:

external-link copy
15 : 79

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Je! Imekufikia hadithi ya Musa? info

Ewe Muhammad! Imekufikilia hadithi ya Musa,

التفاسير:

external-link copy
16 : 79

إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى

Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia: info

Alipo mwita Mola wake Mlezi katika bonde lilio takaswa, linalo itwa "T'uwa"?

التفاسير:

external-link copy
17 : 79

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri info

Akaambiwa: Nenda kwa Firauni aliye pindukia mpaka katika udhalimu.

التفاسير:

external-link copy
18 : 79

فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ

Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa? info

Umwambie: Je! Huelekei kut'ahirika?

التفاسير:

external-link copy
19 : 79

وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ

Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha. info

Na mimi nikuongoze upate kumjua Mola wako Mlezi, umwogope.

التفاسير:

external-link copy
20 : 79

فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi alimwonyesha Ishara kubwa. info

Musa akamwonyesha Firauni miujiza mikubwa.

التفاسير:

external-link copy
21 : 79

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

Lakini aliikadhibisha na akaasi. info

Lakini Firauni alimkadhibisha Musa kwa aliyo kuja nayo, na akamuasi kwa aliyo mwitia.

التفاسير:

external-link copy
22 : 79

ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ

Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi. info

Kisha akamgeuzia mgongo, akenda kujitahidi kumpinga.

التفاسير:

external-link copy
23 : 79

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

Akakusanya watu akanadi. info

Akawakusanya wachawi, na akawaita watu,

التفاسير:

external-link copy
24 : 79

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa. info

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa.

التفاسير:

external-link copy
25 : 79

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ

Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo. info

Mwenyezi Mungu akampa adhabu kwa kauli yake ya mwisho, nayo ni vile kusema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa. Na akampa adhabu kwa kauli yake ya mwanzo, nayo ni kumkadhibisha Musa a.s.

التفاسير:

external-link copy
26 : 79

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ

Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa. info

Hakika katika hadithi hiyo yapo mawaidha kwa mwenye kumkhofu Mwenyezi Mungu.

التفاسير:

external-link copy
27 : 79

ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga! info

Enyi mnao kanya kufufuliwa! Kukuumbeni nyinyi ni taabu zaidi au kuziumba mbingu, kuzikusanya sehemu zake zilio tawanyika mbali mbali,

التفاسير:

external-link copy
28 : 79

رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا

Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri. info

Na kunyanyua kimo chake, na zikakaa sawa hazina tafauti wala ila?

التفاسير:

external-link copy
29 : 79

وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake info

Na akatia kiza katika usiku wake, na akautokeza mchana wake ukawa na mwangaza?

التفاسير:

external-link copy
30 : 79

وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ

Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi. info

Na ardhi baada ya hayo akaikunjua, na akaisawazisha, ikasilihi kukaliwa na watu wake?

التفاسير:

external-link copy
31 : 79

أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake, info

Akatoa ndani yake maji yake yanayo tibuka katika chemchem zake, na ikamiminika mito yake, na ikawa na mimea yake ya chakula kwa ajili ya watu na wanyama;

التفاسير:

external-link copy
32 : 79

وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا

Na milima akaisimamisha, info

Na milima akaithibitisha imara

التفاسير:

external-link copy
33 : 79

مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Kwa nafuu yenu na mifugo yenu. info

Kwa ajili ya manufaa yenu na wanyama wenu mnao wafuga!

التفاسير:

external-link copy
34 : 79

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa, info

Kitakapo fika Kiyama ambacho vitisho vyake vitaenea kote,

التفاسير:

external-link copy
35 : 79

يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya, info

Siku atakapo kumbuka mtu vitendo vyake vya kheri au shari,

التفاسير:

external-link copy
36 : 79

وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona, info

Na Jahannamu ikadhihirishwa wazi, akaiona kila mwenye macho kuwa ndio malipo,

التفاسير:

external-link copy
37 : 79

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

Basi ama yule aliye zidi ujeuri, info

Basi ama mwenye kupita mpaka kwa maasi yake,

التفاسير:

external-link copy
38 : 79

وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Na akakhiari maisha ya dunia, info

Na akajichagulia nafsi yake maisha yanayo pita njia,

التفاسير:

external-link copy
39 : 79

فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake! info

Basi Moto wa Jahannamu unao babua upepo wake ndio makaazi yake wala hana mengineyo.

التفاسير:

external-link copy
40 : 79

وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ

Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio, info

Na ama mwenye kukhofu ukubwa na utukufu wa Mola wake Mlezi, na akaizuia nafsi yake na matamanio ya kumpumbaza,

التفاسير:

external-link copy
41 : 79

فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake! info

Basi huyo nyumba ya neema ya Peponi ndio makaazi yake, wala hana penginepo.

التفاسير:

external-link copy
42 : 79

يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا

Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini? info

Ewe Muhammad! Wanakuuliza, ati, khabari za Saa ya Kiyama, itakuwa lini?

التفاسير:

external-link copy
43 : 79

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ

Una nini wewe hata uitaje? info

Ujuzi wa hayo hauko kwako hata uwatajie.

التفاسير:

external-link copy
44 : 79

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ

Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake. info

Ujuzi wa hayo uko kwa Mola wako Mlezi tu, si kwa mwenginewe. (Nabii Isa a.s. ambaye Wakristo wanasema ni Mwana wa Mungu, au ndiye Mungu, pia anasimuliwa katika Biblia kuwa hakuijua Saa na Siku ya Kiyama. Injili ya Mathayo inanukulu maneno ya Yesu: "Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.")

التفاسير:

external-link copy
45 : 79

إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu. info

Kwani waajibu wako ni kuwaonya wanao khofu si kuwatangazia wakati wake.

التفاسير:

external-link copy
46 : 79

كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا

Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake. info

Na wao siku watakayo iona hiyo Saa ya Kiyama ni kama kwamba hawakuishi duniani zaidi kuliko jioni moja tu, au mchana wake.

التفاسير: