Ameita, mwenye kuita, kuhimiza kama kufanya kejeli, iletwe upesi adhabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu ambayo hapana shaka itawashukia makafiri.
Wala hapana chochote cha kuzuia adhabu hiyo,
Kwani hiyo inatoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu, ambako huko ndiko zinatoka nguvu zinazo simama, na hukumu inayo tekelezwa.
Malaika na Jibrili wanapanda kwenda kunako toka amri yake kwa siku ambayo urefu wake ni miaka khamsini elfu kwa mujibu wa hisabu ya miaka ya duniani.
Basi, ewe Muhammad! Subiri uwastahamilie hizo kejeli zao, na kuhimiza kwao adhabu, kwa subira isiyo kuwa na mbabaiko ndani yake wala mashtaka.
Hakika hao makafiri wanaiona hiyo Siku ya Kiyama ni kitu cha muhali kutokea.
Na Sisi tunaona kuwa ni jambo jepesi katika uweza wetu, wala halina uzito wowote.
Siku mbingu itakapo kuwa kama fedha iliyo yayuka,
Na milima itakapo kuwa kama sufi iliyo tiwa rangi na ikapigwa,
Wala jamaa hamuulizi jamaa yake: Nini hali yako? Kwa sababu kila mmoja kajishughulikia nafsi yake!
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number}
Description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
translation_key: (the key of the currently selected translation)
sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns: json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
Example: https://quranenc.com/api/v1/translation/sura//1
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number}
Description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns: json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
Example: https://quranenc.com/api/v1/translation/aya//1/1