Kisha baada yao tulimtuma Musa na ndugu yake Haruni wende kwa Firauni, mfalme wa Misri na watu wake wakuu makhsusi, kuwaita wamuabudu Mwenyezi Mungu peke yake. Nao waliungwa mkono na hoja zenye nguvu. Firauni na kaumu yake walitakabari wakakataa kuitikia wito wa Musa na Haruni. Kwa kukataa kwao huko wakawa wamefanya makosa makubwa na dhambi.