Watu nawajue kuwa hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kumiliki na Mwenye madaraka makuu juu ya vyote viliomo mbinguni na duniani. Na pia wajue kuwa ahadi yake ni ya kweli. Basi Yeye hashindwi na kitu, na hapana yeyote ataye epuka malipwa yake. Lakini wao wamedanganyika na maisha ya dunia, hawajui hayo kwa ujuzi wa yakini!