Walipozitupa kamba zao na fimbo zao, Mūsā aliwaambia, «Mlivyokuja navyo mkavitupa ni uchawi. Mwenyezi Mungu Ataviondoa mlivyokuja navyo na atavitangua. Hakika Mwenyezi Mungu Hakitengenezi kitendo cha anayetembea katika ardhi ya Mwenyezi Mungu kufanya mambo Anayoyachukia na kufanya uharibifu humo kwa kumuasi.
Na Mwenyezi Mungu Atauimarisha ukweli niliokuja nao kutoka Kwake Ataufanya uwe juu ya ubatilifu wenu kwa maneno Yake na amri Yake, ingawa watu wahalifu wenye kufanya maasia, miongoni mwa jamaa za Fir'awn, wanachukia.
Na hawakumuamini Mūsā, amani imshukiye, pamoja na hoja na dalili alizowaletea, isipokuwa kizazi cha watu wake, Wana wa Isrāīl, hali ya kuwa wao wana uoga na Fir'awn na kundi lake wasiwatese kwa kuwaadhibu na wasiwazuie na Dini yao. Na hakika Fir'awn ni mjeuri mwenye kiburi katika ardhi, na hakika Yeye ni miongoni mwa waliopita mpaka katika ukafiri na uharibifu.
Na akasema Mūsā, «Enyi watu wangu, mkimuamini Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, na mkafuata sheria Yake, kuweni na imani na Yeye na jisalimisheni kwa amri Yake. Na kwa Mwenyezi Mungu jitegemezeni iwapo nyinyi ni wenye kumdhalilikia kwa utiifu.
Watu wa Mūsā walisema kumwambia, «Tumemtegemea Mwenyezi Mungu Peke Yake Asiye na mshirika na tumemwachia Yeye mambo yetu. Ewe Mola wetu, usiwape ushindi juu yetu ikawa ni mtihani kwetu katika Dini yetu, au ikawa ni mtihani kwa makafiri kwa kupata ushindi wakasema: lau wao (wenye kumuamini Mūsā) wako kwenye haki hawangalishindwa.
Na tuliwapelekea wahyi Mūsā na Hārūn kwamba watengezeeni watu wenu katika Misri majumba yenye kuwa ni makao na mahali pa hifadhi pa kukimbilia, na myafanye majumba yenu kuwa ni mahali pa kuswali ndani yake mkiwa na uoga, na tekelezeni Swala za faradhi kwa nyakati zake. Na wape Waumini wenye kumtii Mwenyezi Mungu bishara njema ya nguvu ya ushindi na thawabu nyingi kutoka Kwake, kutakata ni Kwake na kutukuka.
Na Mūsā akasema, «Mola wetu, hakika wewe umempa Fir'awn na watukufu wa watu wake pambo la vitu vya duniani wasikushukuru, na wamejisaidia kwa vitu hivyo katika kupotoa watu na njia Yako. Mola wetu, yageuze Mali yao wasifaidike nayo, na uzipige mhuri nyoyo zao zisipate kuikunjukia Imani, wasiamini mpaka waione adhabu kali iumizayo.»