《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼

external-link copy
58 : 8

وَإِمَّا تَخَافَنَّ مِن قَوۡمٍ خِيَانَةٗ فَٱنۢبِذۡ إِلَيۡهِمۡ عَلَىٰ سَوَآءٍۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡخَآئِنِينَ

Na ukichelea khiana kwa watu fulani basi watupilie ahadi yao kwa usawa. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi makhaini. info

Na ukiona alama za hao watu kutaka kuleta khiana kuvunja maagano yaliyo baina yako na wao, ikate njia yao wasiweze kukukhuni, kwa kuwatangazia wewe kuvunja hayo mapatano, mpaka walijue jambo lako, na wasiweze kukukhuni. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi makhaini, wala haridhii kuwa nyinyi msifike kwa sifa yao.

التفاسير: