《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼

external-link copy
57 : 3

وَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَيُوَفِّيهِمۡ أُجُورَهُمۡۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلظَّٰلِمِينَ

Na ama wale walio amini na wakatenda mema basi Mwenyezi Mungu atawalipa ujira wao kaamili. Na Mwenyezi Mungu hawapendi madhaalimu. info

Na ama walio ongoka kwa uwongofu wa Mwenyezi Mungu, wakatenda vitendo vya kufuata mwendo wa kheri, Mwenyezi Mungu atawapa malipo ya kutosha kwa hizo a'mali zao. Na ndiyo shani yake Mwenyezi Mungu kuwa hawalipi thawabu zake wale wanao pindukia mipaka ya Mwenyezi Mungu wakafanya jeuri ya kutoitikia wito wake na kumtendea wema. Wala hawanyanyulii cheo chao.

التفاسير: