《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼

external-link copy
54 : 3

وَمَكَرُواْ وَمَكَرَ ٱللَّهُۖ وَٱللَّهُ خَيۡرُ ٱلۡمَٰكِرِينَ

Na Makafiri walipanga mipango na Mwenyezi Mungu akapanga mipango, na Mwenyezi Mungu ndiye mbora wa wenye kupanga. info

Ama hao makafiri wapinzani walipanga njama za chini kwa chini kuupiga vita wito (Da'wa) wa Isa. Mwenyezi Mungu alizibat'ilisha njama zao, wasifanikiwe kuyapata waliyo yakusudia. Na Mwenyezi Mungu kwa hikima yake anawashinda watu wote wafanyao hila.

التفاسير: