Ewe Nabii! Tunakusimulia kila namna ya khabari ya Mitume walio pita pamoja na kaumu zao kwa ajili ya kukupa nguvu wewe uweze kubeba mashaka ya Utume. Na katika khabari hizi yamekujia maelezo ya haki unayo ilingania mfano walivyo lingania Mitume walio kutangulia, nayo ni Tawhidi ya kuwa Mwenyezi Mungu ni Mpweke, na kuepuka yale ambayo yanamkasirisha, kama yalivyo wajia mawaidha na mazingatio yanayo wanufaisha Waumini, ili wazidi imani yao, na wanao jitayarisha kwa imani ili waifanyie haraka hiyo imani.