పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అలీ ముహ్సిన్ అల్ బర్వానీ

పేజీ నెంబరు:close

external-link copy
10 : 3

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَن تُغۡنِيَ عَنۡهُمۡ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَلَآ أَوۡلَٰدُهُم مِّنَ ٱللَّهِ شَيۡـٔٗاۖ وَأُوْلَٰٓئِكَ هُمۡ وَقُودُ ٱلنَّارِ

Kwa hakika wale walio kufuru hazitowafaa kitu kwa Mwenyezi Mungu mali zao, wala watoto wao; nao hao ndio kuni za Motoni. info

Katika Siku hiyo makafiri hawatokingwa na mali yao na yangawa mengi vipi, wala na watoto wao na wangawa wengi vipi. Hayo yote yatakuwa ndio kuni za Moto za kuwateketeza wenyewe.

التفاسير:

external-link copy
11 : 3

كَدَأۡبِ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا فَأَخَذَهُمُ ٱللَّهُ بِذُنُوبِهِمۡۗ وَٱللَّهُ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Kama yaliyo wapata watu wa Firauni na wale walio kuwa kabla yao. Walikanusha Ishara zetu, basi Mwenyezi Mungu aliwashika kwa madhambi yao; na Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu. info

Na hali ya hao ni kama hali ya kaumu ya Firauni walio kuwa na inda kabla yao. Walizikadhibisha Ishara za Mwenyezi Mungu juu ya kuwa zilikuwa ziwazi kabisa. Basi Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa sababu ya madhambi waliyo yatenda. Na Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.

التفاسير:

external-link copy
12 : 3

قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ سَتُغۡلَبُونَ وَتُحۡشَرُونَ إِلَىٰ جَهَنَّمَۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ

Waambie walio kufuru: Karibuni mtashindwa na mtakusanywa, mtiwe kwenye Jahannam; nako huko ni makao mabaya kabisa. info

Ewe Nabii! Waambie hawa walio kufuru: Bila ya shaka nyinyi mtashindwa hapa duniani, na kesho Akhera mtaadhibiwa. Na Jahannamu ndio itakuwa tandiko lenu la kulalia; na ovu lilioje tandiko hilo!

التفاسير:

external-link copy
13 : 3

قَدۡ كَانَ لَكُمۡ ءَايَةٞ فِي فِئَتَيۡنِ ٱلۡتَقَتَاۖ فِئَةٞ تُقَٰتِلُ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَأُخۡرَىٰ كَافِرَةٞ يَرَوۡنَهُم مِّثۡلَيۡهِمۡ رَأۡيَ ٱلۡعَيۡنِۚ وَٱللَّهُ يُؤَيِّدُ بِنَصۡرِهِۦ مَن يَشَآءُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّأُوْلِي ٱلۡأَبۡصَٰرِ

Hakika ilikuwa ni Ishara kwenu katika yale majeshi mawili yalipo pambana. Jeshi moja likipigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na jingine kafiri likiwaona zaidi kuliko wao mara mbili, kwa kuona kwa macho. Na Mwenyezi Mungu humuunga mkono amtakaye kwa nusura yake. Hakika katika hayo yapo mazingatio kwa wenye macho. info

Ilikuwa Ishara wazi na mazingatio yaliyo dhaahiri katika makundi mawili ya wapiganaji walipo pambana siku ya Badri. Kundi moja, hilo la Waumini, likipigana kwa ajili ya kutukuza Neno la Mwenyezi Mungu na kueneza Haki. Na kundi la pili, hilo la makafiri, likipigania pumbao na matamanio. Ikawa, basi, Mwenyezi Mungu katika kuwaunga mkono Waumini aliwafanya wale makafiri wawaone Waumini idadi yao mara mbili kuliko walivyo. Kwa hivyo makafiri wakaingiwa na khofu nyoyoni mwao wakaemewa. Na Mwenyezi Mungu humnusuru amtakaye. Katika haya, hakika, pana mazingatio kwa wenye nadhari iliyo ongoka isiyo kengeuka na kuiacha Haki.

التفاسير:

external-link copy
14 : 3

زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ ٱلشَّهَوَٰتِ مِنَ ٱلنِّسَآءِ وَٱلۡبَنِينَ وَٱلۡقَنَٰطِيرِ ٱلۡمُقَنطَرَةِ مِنَ ٱلذَّهَبِ وَٱلۡفِضَّةِ وَٱلۡخَيۡلِ ٱلۡمُسَوَّمَةِ وَٱلۡأَنۡعَٰمِ وَٱلۡحَرۡثِۗ ذَٰلِكَ مَتَٰعُ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَٱللَّهُ عِندَهُۥ حُسۡنُ ٱلۡمَـَٔابِ

Watu wamepambiwa kupenda matamanio ya wanawake, na wana, na mirundi ya dhahabu na fedha, na farasi asili, na mifugo, na mashamba. Hayo ni starehe ya maisha ya duniani; na kwa Mwenyezi Mungu ndio kwenye marejeo mema. info

Wanaadamu wameumbwa kuwa wanapenda matamanio ya vitu kama wanawake, wana, na wingi wa madhahabu na fedha, na farasi wazuri wazuri walio fundishika, na mifugo kama ngamia, ng'ombe, mbuzi, kondoo, na kadhaalika mashamba makubwa. Lakini yote hayo ni starehe na kwa matumizi ya uhai huu wa duniani wenye kupita na kuondoka. Na hayo si chochote si lolote ukilinganisha na hisani anayo wafanyia Mwenyezi Mungu waja wake wanao pigania jihadi katika Njia yake watakapo rejea kwake Yeye Akhera.

التفاسير:

external-link copy
15 : 3

۞ قُلۡ أَؤُنَبِّئُكُم بِخَيۡرٖ مِّن ذَٰلِكُمۡۖ لِلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا وَأَزۡوَٰجٞ مُّطَهَّرَةٞ وَرِضۡوَٰنٞ مِّنَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ

Sema: Nikwambieni yaliyo bora kuliko hayo? Kwa wachamngu ziko Bustani kwa Mola wao zipitazo mito kati yake. Watadumu humo, na wake walio takaswa, na wanazo radhi za Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake. info

Ewe Nabii! Sema: Nikwambieni yaliyo bora kuliko hayo yote mliyo pambiwa duniani? Kwa wale wachamngu wamewekewa malipo ya dhamana kwa Mola wao Mlezi, nayo ni Bustani zipitazo mito chini ya vivuli vya miti. Humo watastarehe kwa maisha mazuri wala hawatoingiliwa na khofu ya kuwa neema hiyo itaondoka, kwani wamekwisha katibiwa kuwa humo watabaki daima milele. Watakuwamo humo wake walio t'ahirika, wamesafika na kila ila ya wanawake wa kidunia. Na juu ya yote hayo, watapata Radhi ya Mwenyezi Mungu ambayo wataihisi chini ya kivuli chake kuwa ndiyo Neema kubwa kabisa. Na Mwenyezi Mungu anazijua vyema hali za waja wake; hapana jambo linalo fichikana kwake, hawana siri asiyo ijua Yeye.

التفاسير: