పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ మరియు నాసర్ ఖమీస్

పేజీ నెంబరు:close

external-link copy
53 : 6

وَكَذَٰلِكَ فَتَنَّا بَعۡضَهُم بِبَعۡضٖ لِّيَقُولُوٓاْ أَهَٰٓؤُلَآءِ مَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنۢ بَيۡنِنَآۗ أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَعۡلَمَ بِٱلشَّٰكِرِينَ

Na hivyo basi Mwenyezi Mungu Amewapa mtihani waja Wake kwa kutafautiana mafungu yao ya riziki na umbo, Akawafanya baadhi yao matajiri na wengine maskini, baadhi yao wenye nguvu na wengine madhaifu Na Akawafanya baadhi yao ni wahitaji wa wengine ili kuwajaribu kwa hilo, wapate makafiri matajiri kusema, «Ni madhaifu hawa, miongoni mwetu, Mwenyezi Mungu Amewapa neema ya Uislamu?» Kwani Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, si Mjuzi zaidi wa wanaoshukuru neema Yake Akawaafikia kwenye uongofu wa dini Yake? info
التفاسير:

external-link copy
54 : 6

وَإِذَا جَآءَكَ ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِنَا فَقُلۡ سَلَٰمٌ عَلَيۡكُمۡۖ كَتَبَ رَبُّكُمۡ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَ أَنَّهُۥ مَنۡ عَمِلَ مِنكُمۡ سُوٓءَۢا بِجَهَٰلَةٖ ثُمَّ تَابَ مِنۢ بَعۡدِهِۦ وَأَصۡلَحَ فَأَنَّهُۥ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na wakikujia, ewe Nabii, wale wanaoamini aya za Mwenyezi Mungu zenye kushuhudia ukweli wako juu ya Qur’ani na mengineyo, kutaka fatuwa kuhusu toba ya madhambi yao yaliyotangulia, basi wakirimu kwa kuwarudishia salamu na uwape bishara ya rehema ya Mwenyezi Mungu iliyo kunjufu. Kwani Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, Ametoa ahadi Yake Mwenyewe kuwarehemu waja Wake kwa kuwafanyia wema kwamba mwenye kufanya dhambi kwa kutojua mwisho wake mbaya na kuwa linapelekea kukasirikiwa na Mwenyezi Mungu-Basi kila mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu kwa kukosea au kwa kusudi huwa ni mjinga kwa mtizamo huu, ingawa ajua kuwa ni haramu- kisha baada yake akatubia na akaendelea kufanya matendo mema, basi Mwenyezi Mungu Atamsamehe dhambi lake, kwani Yeye ni Mwingi wa kusamehe kwa waja Wake wenye kutubia, ni Mwingi wa rehema kwao. info
التفاسير:

external-link copy
55 : 6

وَكَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ وَلِتَسۡتَبِينَ سَبِيلُ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Na mfano wa ufafanuzi huu tuliokufafanulia, tunakufafanulia, ewe Mtume, hoja zilizo wazi kwa kila mtu, ili ifunuke njia ya watu wa haki wanayoikanusha watu wa batili, na ifunuke njia ya watu wa batili wenye kuwaendea kinyume Mitume. info
التفاسير:

external-link copy
56 : 6

قُلۡ إِنِّي نُهِيتُ أَنۡ أَعۡبُدَ ٱلَّذِينَ تَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِۚ قُل لَّآ أَتَّبِعُ أَهۡوَآءَكُمۡ قَدۡ ضَلَلۡتُ إِذٗا وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُهۡتَدِينَ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, Amenikataza niabudu masanamu ambao mnaowaabudu badala Yake.» Na uwaambie, «Sitafuata matamanio yenu. Nitakuwa nimepotea njia ya sawa nikifuata matamanio yenu na sitakuwa ni miongoni mwa walioongoka.» info
التفاسير:

external-link copy
57 : 6

قُلۡ إِنِّي عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّي وَكَذَّبۡتُم بِهِۦۚ مَا عِندِي مَا تَسۡتَعۡجِلُونَ بِهِۦٓۚ إِنِ ٱلۡحُكۡمُ إِلَّا لِلَّهِۖ يَقُصُّ ٱلۡحَقَّۖ وَهُوَ خَيۡرُ ٱلۡفَٰصِلِينَ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Mimi niko kwenye hoja iliyo wazi ya sheria ya Mwenyezi Mungu Aliyoniletea kwa njia ya wahyi. Nayo ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu Peke Yake kwa ibada. Na hili mlilikanusha. Na haliko kwenye uwezo wangu jambo la kuwateremshia adhabu mnayoitaka kwa haraka. Na uamuzi wa kuchelewesha hilo uko tu kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka. Yeye Anahadithia ukweli na Yeye Ndiye bora wa kupambanua baina ya haki na batili kwa uamuzi Wake na hukumu Yake.» info
التفاسير:

external-link copy
58 : 6

قُل لَّوۡ أَنَّ عِندِي مَا تَسۡتَعۡجِلُونَ بِهِۦ لَقُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۗ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِٱلظَّٰلِمِينَ

Sema, ewe Mtume, «Lau mimi nina mamlaka ya kuwateremshia adhabu ambayo mnaitaka kwa haraka, ningaliiteremsha kwenu, na uamuzi, baina yangu mimi na nyinyi, ungalitoka. Lakini hilo liko kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka. Na Yeye Anawajua zaidi madhalimu ambao wamepita mipaka yao wakawashirikisha wengine pamoja na Yeye. info
التفاسير:

external-link copy
59 : 6

۞ وَعِندَهُۥ مَفَاتِحُ ٱلۡغَيۡبِ لَا يَعۡلَمُهَآ إِلَّا هُوَۚ وَيَعۡلَمُ مَا فِي ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِۚ وَمَا تَسۡقُطُ مِن وَرَقَةٍ إِلَّا يَعۡلَمُهَا وَلَا حَبَّةٖ فِي ظُلُمَٰتِ ٱلۡأَرۡضِ وَلَا رَطۡبٖ وَلَا يَابِسٍ إِلَّا فِي كِتَٰبٖ مُّبِينٖ

Na kwa Mwenyezi Mungu , Aliyetukuka na kuwa juu, kuna mafātih( al-ghayb, yaani: hazina za mambo ya ghaibu yaliyofichika, hakuna azijuwazo ila Yeye. Miongoni mwazo ni ujuzi wa Kiyama, kuteremka mvua, viliyomo ndani ya zao, matendo ya siku zinazokuja na mahala mtu atakapokufa. Na Anajua kila kilichoko barani na baharini. Na hakuna jani, linaloanguka kutoka kwenye mmea wowote, isipokuwa Yuwalijua. Na kila chembe iliyofichika ardhini na kila kibichi na kikavu, kimethibitishwa kwenye kitabu kilicho wazi kisicho na utatizi nacho ni Al-Lawh(Al-Maḥfūẓ ( Ubao Uliohifadhiwa) info
التفاسير: