పవిత్ర ఖురాన్ యొక్క భావార్థాల అనువాదం - స్వాహిలి అనువాదం - అబ్దుల్లాహ్ ముహమ్మద్ మరియు నాసర్ ఖమీస్

పేజీ నెంబరు: 119:106 close

external-link copy
71 : 5

وَحَسِبُوٓاْ أَلَّا تَكُونَ فِتۡنَةٞ فَعَمُواْ وَصَمُّواْ ثُمَّ تَابَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ ثُمَّ عَمُواْ وَصَمُّواْ كَثِيرٞ مِّنۡهُمۡۚ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Na walidhania waasi hawa kwamba Mwenyezi Mungu Hatawatia mkononi kwa kuwaadhibu kwa sababu ya kuasi kwao na kutakabari kwao, ndipo wakaendelea katika matamanio yao na wakawa vipofu wa kutouona uongofu na wakawa viziwi wa kutoisikia na kutonufaika na haki. Hapo Mwenyezi Mungu Aliwateremshia adhabu Yake, wakatubia na Mwenyezi Mungu Akawakubalia toba zao. Kisha wengi wao walikuwa vipofu na viziwi baada ya kubainikiwa na haki. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona matendo yao, mazuri na mabaya, na Atawalipa kwa matendo yao hayo. info
التفاسير:

external-link copy
72 : 5

لَقَدۡ كَفَرَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡمَسِيحُ ٱبۡنُ مَرۡيَمَۖ وَقَالَ ٱلۡمَسِيحُ يَٰبَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ رَبِّي وَرَبَّكُمۡۖ إِنَّهُۥ مَن يُشۡرِكۡ بِٱللَّهِ فَقَدۡ حَرَّمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ ٱلۡجَنَّةَ وَمَأۡوَىٰهُ ٱلنَّارُۖ وَمَا لِلظَّٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٖ

Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anaapa kwamba wale ambao walisema, «Mwenyezi Mungu Ndiye al-Masīh, mwana wa Maryam,» wameshakufuru kwa maneno yao haya. Na Alitoa habari Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kwamba al- Masīh, alisema kuwaambia Wana wa Isrāīl, «Muabuduni Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Asiye na mshirika, kwani mimi na nyinyi katika uja tuko sawa.» Kwa hakika, yoyote atakayemuabudu mwengine, pamoja na Mwenyezi Mungu, Aliye Pweke, basi Mwenyezi Mungu Ataifanya Pepo kuwa ni haramu kwake na Ataufanya Moto kuwa ndio makao yake na hatakuwa na msaidizi wa kumuokoa nao Moto huo. info
التفاسير:

external-link copy
73 : 5

لَّقَدۡ كَفَرَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ ثَالِثُ ثَلَٰثَةٖۘ وَمَا مِنۡ إِلَٰهٍ إِلَّآ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞۚ وَإِن لَّمۡ يَنتَهُواْ عَمَّا يَقُولُونَ لَيَمَسَّنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ

Hakika wamekufuru Wanaswara waliosema, «Mwenyezi Mungu ni mkusanyiko wa vitu vitatu: Baba, Mwana na Roho mtakatifu.» Kwani Wanaswara hawa hawakujua kwamba watu hawana isipokuwa muabudiwa Mmoja, Hakuzaa wala Hakuzaliwa? Na iwapo wenye kusema maneno haya hawatakoma na uzushi wao na urongo wao, hakika itawapata wao adhabu iliyo kali iumizayo kwa sababu ya kumkufuru kwao Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
74 : 5

أَفَلَا يَتُوبُونَ إِلَى ٱللَّهِ وَيَسۡتَغۡفِرُونَهُۥۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Mbona Wanaswara hawa hawarudi kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na wakatubia kwa waliyoyasema na wakamuomba msamaha Mwenyezi Mungu Aliyetukuka? Kwani Mwenyezi Mungu , Aliyetukuka, ni Mwenye kuyasamehe madhambi ya wenye kutubia, ni Mwenye huruma kwao. info
التفاسير:

external-link copy
75 : 5

مَّا ٱلۡمَسِيحُ ٱبۡنُ مَرۡيَمَ إِلَّا رَسُولٞ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِهِ ٱلرُّسُلُ وَأُمُّهُۥ صِدِّيقَةٞۖ كَانَا يَأۡكُلَانِ ٱلطَّعَامَۗ ٱنظُرۡ كَيۡفَ نُبَيِّنُ لَهُمُ ٱلۡأٓيَٰتِ ثُمَّ ٱنظُرۡ أَنَّىٰ يُؤۡفَكُونَ

Hakuwa al-Masih, mwana Maryam isipokuwa ni Mtume kama wale Mitume waliomtangulia; na mamake aliamini Imani ya dhati, kiilimu na kivitendo. Na wote wawili wanahitajia chakula kama walivyo binadamu wengineo. Na anayehitaji chakula ili aishi, hawi ni mungu. Basi izingatie, ewe Mtume, hali ya hawa makafiri.Tumekufafanulia alama zinazoonyesha upweke wetu na ubatilifu wa yale wanayoyadai kuhusu Mitume wa Mwenyezi Mungu. Kisha wao, pamoja na hilo, wanapotea njia ya haki ambayo sisi tunawaongoza waifuate. Kisha hebu angalia, vipi wanaepushwa na haki baada ya ufafanuzi huu? info
التفاسير:

external-link copy
76 : 5

قُلۡ أَتَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَمۡلِكُ لَكُمۡ ضَرّٗا وَلَا نَفۡعٗاۚ وَٱللَّهُ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia makafiri hawa, «Vipi mtamshirikisha Mwenyezi Mungu na asiyeweza kuwadhuru chochote wala kuwaletea manufaa yoyote?» Mwenyezi Mungu Ndiye Mwenye kuyasikia maneno ya waja Wake, Ndiye Mwenye kuzijua hali zao. info
التفاسير:

external-link copy
77 : 5

قُلۡ يَٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لَا تَغۡلُواْ فِي دِينِكُمۡ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ وَلَا تَتَّبِعُوٓاْ أَهۡوَآءَ قَوۡمٖ قَدۡ ضَلُّواْ مِن قَبۡلُ وَأَضَلُّواْ كَثِيرٗا وَضَلُّواْ عَن سَوَآءِ ٱلسَّبِيلِ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia Wanaswara, «Msiikiuke haki katika yale mnayoyaamini kuhusu mambo ya al-Masih. Wala msifuate matamanio yenu kama Mayahudi walivyofuata matamanio yao katika mambo ya dini, wakaingia kwenye upotevu, wakawafanya watu wengi wamkanushe Mwenyezi Mungu na wakatoka kwenye njia nyofu, wakaifuata njia ya upotovu na upotevu. info
التفاسير: