[1] Aya hii inawaonya wana wa Israili dhidi ya kuyauza mafundisho ya Mwenyezi Mungu kwa kuficha maelezo ya Muhammad - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - yaliyopo katika vitabu vyao. Na kuchukua "thamani ndogo" ya duniani kama vile yale wanayopata kutoka kwa wafuasi wao kama vile chakula, uongozi n.k. (Tafsir Al-Wajiiz cha Al-Waahidii)