د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - علی محسن البرواني

د مخ نمبر:close

external-link copy
55 : 16

لِيَكۡفُرُواْ بِمَآ ءَاتَيۡنَٰهُمۡۚ فَتَمَتَّعُواْ فَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ

Wakizikataa neema tulizo wapa. Basi stareheni. Mtakuja jua! info

Hayo hutokea ili mwisho wao huwa kuikanya fadhila yetu kwa yale tuliyo wapa. Basi enyi makafiri! Stareheni na hayo msiyo yatolea Haki ya shukrani. Mtakuja kuujua mwisho wa ukafiri!

التفاسير:

external-link copy
56 : 16

وَيَجۡعَلُونَ لِمَا لَا يَعۡلَمُونَ نَصِيبٗا مِّمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡۗ تَٱللَّهِ لَتُسۡـَٔلُنَّ عَمَّا كُنتُمۡ تَفۡتَرُونَ

Na hao ambao hata hawawajui wanawawekea sehemu ya tunavyo waruzuku.Wallahi! Bila ya shaka mtasailiwa kwa hayo mliyo kuwa mnayazua! info

Na washirikina huyapa masanamu yao, ambayo wanayaita kwa ujinga wao kuwa ni miungu, sehemu ya kujikaribisha kwayo kutokana na zile riziki tulizo wapa Sisi, katika makulima na mifugo na vyenginevyo. Nakuulizeni, kwa Utukufu wangu, enyi washirikina, hayo mliyo khitalifiana kwayo katika uwongo wenu na upotovu mlio uzua. Na Mimi nitakulipeni kwayo.

التفاسير:

external-link copy
57 : 16

وَيَجۡعَلُونَ لِلَّهِ ٱلۡبَنَٰتِ سُبۡحَٰنَهُۥ وَلَهُم مَّا يَشۡتَهُونَ

Na wanamfanyia Mwenyezi Mungu ati ana mabinti, Subhanahu, Aliyetakasika! Na wao wenyewe, ati ndio wawe na hayo wanayo yatamani! info

Na hujaalia kumpa Mwenyezi Mungu yale wayachukiayo wao, kwa kudai kuwa Malaika ni watoto wake wa kike, na wao wanawaabudu. Mwenyezi Mungu apishe mbali na hayo! Na wao ati wanajipa wayapendayo nayo ni watoto wanaume.

التفاسير:

external-link copy
58 : 16

وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُم بِٱلۡأُنثَىٰ ظَلَّ وَجۡهُهُۥ مُسۡوَدّٗا وَهُوَ كَظِيمٞ

Na mmoja wao akibashiriwa kwa msichana, uso wake unasawijika,naye kajaa chuki. info

Na akiambiwa mmoja wao kwamba amepata mtoto wa kike, uso wake unasawijika kwa huzuni, naye amejaa hasira na amekasirika.

التفاسير:

external-link copy
59 : 16

يَتَوَٰرَىٰ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ مِن سُوٓءِ مَا بُشِّرَ بِهِۦٓۚ أَيُمۡسِكُهُۥ عَلَىٰ هُونٍ أَمۡ يَدُسُّهُۥ فِي ٱلتُّرَابِۗ أَلَا سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ

Anajificha asionekane na watu kwa ubaya wa aliyo bashiriwa! Je,akae naye juu ya fedheha hiyo au amfukie udongoni? Tazama uovu wa wanavyohukumu! info

Anajaribu kujificha watu wasiione huzuni ya machungu yaliyo mpata kwa kupewa khabari ya binti aliye zaliwa. Anatapatapa: amwache hai juu ya fedheha anayo iona, kama anavyo jigamba? Au amzike katika udongo naye yuhai mpaka afe? Ewe msikilizaji! Zingatia uwovu wa vitendo vya watu hawa! Na uovu gani wa kumhukumia Mwenyezi Mungu mabinti ambao wao wanawachukia!

التفاسير:

external-link copy
60 : 16

لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ مَثَلُ ٱلسَّوۡءِۖ وَلِلَّهِ ٱلۡمَثَلُ ٱلۡأَعۡلَىٰۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Hali ya wasio iamini Akhera ni ovu; na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye sifa tukufu. Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima. info

Ni hali mbaya ya wasio amini Akhera na yote yaliyoko huko ya thawabu na adhabu, nayo ni ile haja ya kutaka watoto wa kiume na kuchukia watoto wa kike. Na Mwenyezi Mungu ana sifa tukufu. Yeye ni Mkwasi, hahitajii kitu, wala hana haja ya mtoto. Naye ni Mwenye kushinda, Mwenye nguvu, wala hana haja ya msaidizi.

التفاسير:

external-link copy
61 : 16

وَلَوۡ يُؤَاخِذُ ٱللَّهُ ٱلنَّاسَ بِظُلۡمِهِم مَّا تَرَكَ عَلَيۡهَا مِن دَآبَّةٖ وَلَٰكِن يُؤَخِّرُهُمۡ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗىۖ فَإِذَا جَآءَ أَجَلُهُمۡ لَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ سَاعَةٗ وَلَا يَسۡتَقۡدِمُونَ

Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli wachukulia watu kwa mujibu wa dhulma zao, basi asingeli mwacha hapa hata mnyama mmoja. Lakini anawaakhirisha mpaka muda ulio wekwa. Na unapo fika muda wao hawatakawilia hata saa moja wala hawatatangulia. info

Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli fanya haraka kuwaadhibu watu kwa dhulma zao wanazo zifanya, basi asingeli mwacha hata mnyama mmoja juu ya ardhi. Lakini Yeye kwa upole wake na hikima yake anawaakhirisha madhaalimu mpaka wakati aliyo uweka, nao ndio wakati utapo kwisha muda wao. Ukija wakati huo hawato taakhari hata kidogo, wala hawato tangulia.

التفاسير:

external-link copy
62 : 16

وَيَجۡعَلُونَ لِلَّهِ مَا يَكۡرَهُونَۚ وَتَصِفُ أَلۡسِنَتُهُمُ ٱلۡكَذِبَ أَنَّ لَهُمُ ٱلۡحُسۡنَىٰۚ لَا جَرَمَ أَنَّ لَهُمُ ٱلنَّارَ وَأَنَّهُم مُّفۡرَطُونَ

Na wanampa Mwenyezi Mungu wanavyo vichukia wao, na ndimi zao zinasema uwongo kwamba wao watapata mema. Hapana shaka hakika wamewekewa Moto, nao wataachwa humo. info

Na washirikina wanamnasibisha Mwenyezi Mungu mabinti na ushirika mambo ambayo wao wanayachukia. Na ndimi zao zinatamka uwongo wanapo dai ya kwamba, kama walivyo kuwa na utajiri na utawala duniani, basi kadhaalika Akhera nao watapata malipo mema kwa Mwenyezi Mungu watapo fufuliwa; nayo ni Pepo! Hapana shaka hao watatiwa Motoni, nao watasukumwa huko kabla ya wengineo.

التفاسير:

external-link copy
63 : 16

تَٱللَّهِ لَقَدۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَىٰٓ أُمَمٖ مِّن قَبۡلِكَ فَزَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَعۡمَٰلَهُمۡ فَهُوَ وَلِيُّهُمُ ٱلۡيَوۡمَ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Wallahi! Sisi tulituma Mitume kwa umati zilizo kuwa kabla yako,lakini Shetani aliwapambia vitendo vyao. Kwa hivyo leo yeye ndiye rafiki yao; nao watapata adhabu chungu. info

Ewe Nabii! Jua kwa yakini kwamba Sisi tuliwatuma Mitume kabla yako kwa kaumu nyingi kama tulivyo kutuma wewe kwa watu wote. Lakini Shetani aliwapambia ukafiri, na ushirikina, na maasi. Basi wakawakanya Mitume wao, na wakawaasi, na wakamsadiki Shetani na wakamt'ii yeye. Basi yeye amekuwa ndiye mwenye kuyatawala mambo yao katika dunia, akiwapambia mambo ya kuwadhuru. Na Akhera watapata adhabu yenye machungu makali.

التفاسير:

external-link copy
64 : 16

وَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّا لِتُبَيِّنَ لَهُمُ ٱلَّذِي ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٗ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ

Na hatukukuteremshia Kitabu isipo kuwa uwabainishie yale ambayo wanakhitalifiana, na kiwe Uwongofu na Rehema kwa watu wanao amini. info

Na hatukukuteremshia wewe hii Qur'ani isipo kuwa upate kuwabainishia watu haki katika yale waliokhitalifiana kwayo katika dini, na ili ipate kuwa ni uwongofu ulio timia na rehema ilio enea kwa kaumu yenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Kitabu alicho kiteremsha.

التفاسير: