ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫

ߞߐߜߍ ߝߙߍߕߍ:close

external-link copy
131 : 6

ذَٰلِكَ أَن لَّمۡ يَكُن رَّبُّكَ مُهۡلِكَ ٱلۡقُرَىٰ بِظُلۡمٖ وَأَهۡلُهَا غَٰفِلُونَ

Ili asiadhibiwe yoyote kwa kujidhulumu nafsi yake kwa kufanya maovu na hali ulinganizi wa Uislamu haujamfikia, sisi tulituma Mitume na tukateremsha Vitabu kwa kuwaondolea majini na binadamu hoja watakayoichukua kama kisingizio. Hivyo ndivyo tulivyowaondolea hoja umma waliyopita, hatukumuadhibu yoyote isipokuwa baada ya kuwapelekea Mitume. info
التفاسير:

external-link copy
132 : 6

وَلِكُلّٖ دَرَجَٰتٞ مِّمَّا عَمِلُواْۚ وَمَا رَبُّكَ بِغَٰفِلٍ عَمَّا يَعۡمَلُونَ

Na kila mwenye kufanya vitendo vya kumtii Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, vya kumuasi ana daraja kutokana na vitendo vyake, Mwenyezi Mungu Atamfikishia viwango hivyo na Atamlipa kwavyo. Na Mola wako, ewe Mtume, Hakuwa ni Mwenye kughafilika na wanayoyafanya waja Wake. info
التفاسير:

external-link copy
133 : 6

وَرَبُّكَ ٱلۡغَنِيُّ ذُو ٱلرَّحۡمَةِۚ إِن يَشَأۡ يُذۡهِبۡكُمۡ وَيَسۡتَخۡلِفۡ مِنۢ بَعۡدِكُم مَّا يَشَآءُ كَمَآ أَنشَأَكُم مِّن ذُرِّيَّةِ قَوۡمٍ ءَاخَرِينَ

Na Mola wako, ewe Mtume, Aliyewaamrisha watu kumuabudu, Ndiye Mkwasi Peke Yake, na viumbe wote wanamhitajia Yeye. Na Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Mwenye rehema kunjufu. Na lau Alitaka Angaliwaangamiza na Akawaleta watu wengine wasiokuwa nyinyi watakaokuwa badala yenu baada ya kumalizika kwenu na watende matendo ya kumtii Yeye, Aliyetukuka, kama Alivyowaleta nyinyi kutokamana na kizazi cha watu wengine waliokuwako kabla yenu. info
التفاسير:

external-link copy
134 : 6

إِنَّ مَا تُوعَدُونَ لَأٓتٖۖ وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ

Hakika yale mateso ambayo Anawaahidi nayo Mola wenu, enyi washirikina, kwa ukafiri wenu, ni yenye kuwapata. Na hamutamlemea Mola wenu kwa kumkimbia. Kwani Yeye ana uwezo wa kuwarudisha, hata kama mtakuwa mumegeuka mumekuwa mchanga na mifupa. info
التفاسير:

external-link copy
135 : 6

قُلۡ يَٰقَوۡمِ ٱعۡمَلُواْ عَلَىٰ مَكَانَتِكُمۡ إِنِّي عَامِلٞۖ فَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ مَن تَكُونُ لَهُۥ عَٰقِبَةُ ٱلدَّارِۚ إِنَّهُۥ لَا يُفۡلِحُ ٱلظَّٰلِمُونَ

Sema, ewe Mtume, «Enyi watu wangu, fanyeni kwa njia yenu, na mimi nitafanya kwa njia yangu ambayo Mola wangu, Aliyetukuka na kuwa juu, Aliniwekea. Mtakuja kujua, pindi mateso yatakapowashukia, ni nani atakayekuwa na mwisho mwema?» Hakika hatafaulu kupata radhi za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na Pepo yule aliyekiuka mpaka Wake na akadhulumu, na akamshirikisha pamoja na Mwenyezi Mungu asiyekuwa Yeye. info
التفاسير:

external-link copy
136 : 6

وَجَعَلُواْ لِلَّهِ مِمَّا ذَرَأَ مِنَ ٱلۡحَرۡثِ وَٱلۡأَنۡعَٰمِ نَصِيبٗا فَقَالُواْ هَٰذَا لِلَّهِ بِزَعۡمِهِمۡ وَهَٰذَا لِشُرَكَآئِنَاۖ فَمَا كَانَ لِشُرَكَآئِهِمۡ فَلَا يَصِلُ إِلَى ٱللَّهِۖ وَمَا كَانَ لِلَّهِ فَهُوَ يَصِلُ إِلَىٰ شُرَكَآئِهِمۡۗ سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ

Na wale wenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, waliziweka kando sehemu ya vitu Alivyoviumba miongoni mwa mazao, matunda na wanyama howa wakawapatia wageni na maskini; na wakaziweka kando sehemu nyingine za vitu hivi kwa washirika wao, miongoni mwa masanamu na mizimu. Basi zile zilizotengewa washirika wao zafikishwa kwao peke yao, na hazifiki kwa Mwenyezi Mungu; na zile zilizotengewa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, zinafika kwa washirika wao. Ni mbaya ulioje uaumuzi wa hao watu na kigawanyo chao. info
التفاسير:

external-link copy
137 : 6

وَكَذَٰلِكَ زَيَّنَ لِكَثِيرٖ مِّنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ قَتۡلَ أَوۡلَٰدِهِمۡ شُرَكَآؤُهُمۡ لِيُرۡدُوهُمۡ وَلِيَلۡبِسُواْ عَلَيۡهِمۡ دِينَهُمۡۖ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَا فَعَلُوهُۖ فَذَرۡهُمۡ وَمَا يَفۡتَرُونَ

Na kama ambavyo mashetani waliwapambia washirikina wamtengee Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, katika mazao na wanyama howa, fungu maalumu na fungu kwa washirika wao, vilevile mashetani wamewapambia wengi kati ya washirikina kuwaua watoto wao kwa kuchelea ufukara, ili wawaingize wazazi hawa kwenye maangamivu kwa kuziua nafsi ambazo Mwenyezi Mungu Ameharamisha kuuliwa isipokuwa kwa haki, na ili wawavurugie dini yao iwachanganyikie wapate kupotea na waangamie. Na lau Angalitaka Mwenyezi Mungu wasiifanye hilo hawangalilifanya, lakini Yeye Amelikadiria liwe kwa kujua Kwake uovu wa hali yao na marejeo yao. Basi waache, ewe Mtume, na mambo yao, katika yale ya urongo wanayoyazua , na Mwenyezi Mungu Atahukumu baina yako na wao. info
التفاسير: