ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫

ߞߐߜߍ ߝߙߍߕߍ:close

external-link copy
12 : 41

فَقَضَىٰهُنَّ سَبۡعَ سَمَٰوَاتٖ فِي يَوۡمَيۡنِ وَأَوۡحَىٰ فِي كُلِّ سَمَآءٍ أَمۡرَهَاۚ وَزَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِمَصَٰبِيحَ وَحِفۡظٗاۚ ذَٰلِكَ تَقۡدِيرُ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡعَلِيمِ

Mwenyezi Mungu Akapitisha kuziumba mbingu saba na kuzisawazisha kwa Siku mbili. Na kwa hilo ukatimia uumbaji wa mbingu na ardhi kwa Siku sita kwa hekima Anayoijua Mwenyezi Mungu, pamoja na uweza Wake, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, wa kuziumba kwa mara moja. Na Akapeleka wahyi katika kila uwingu kwa Analolitaka na kuliamuru. Na tumeupamba uwingu wa karibu kwa nyota zinazong’ara na kwa ajili ya kuuhifadhi na Mashetani wanaosikiliza kwa kuiba. Uumbaji huo mzuri ni makadirio ya Aliye Mshindi katika ufalme Wake, Aliye Mjuzi Ambaye ujuzi Wake umekizunguka kila kitu info
التفاسير:

external-link copy
13 : 41

فَإِنۡ أَعۡرَضُواْ فَقُلۡ أَنذَرۡتُكُمۡ صَٰعِقَةٗ مِّثۡلَ صَٰعِقَةِ عَادٖ وَثَمُودَ

Basi wakipuuza wakanushaji hawa baada ya kubainishiwa sifa za Qur’ani zinazotajika vyema, na sifa za Mungu Mkubwa, waambie, «Kwa kweli, ninawaonya nyinyi adhabu yenye kuwamaliza mfano wa adhabu (iliyowashukia watu wa kabila la) 'Ād na Thmud walipomkanusha Mola wao na kuwaasi Mitume wao.» info
التفاسير:

external-link copy
14 : 41

إِذۡ جَآءَتۡهُمُ ٱلرُّسُلُ مِنۢ بَيۡنِ أَيۡدِيهِمۡ وَمِنۡ خَلۡفِهِمۡ أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّا ٱللَّهَۖ قَالُواْ لَوۡ شَآءَ رَبُّنَا لَأَنزَلَ مَلَٰٓئِكَةٗ فَإِنَّا بِمَآ أُرۡسِلۡتُم بِهِۦ كَٰفِرُونَ

Walipowajia Mitume hao kina 'Ād na Thamūd, hawa baada ya wengine wakifuatana, wakiwaamrisha kumuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake Asiyekuwa na mshirika, waliwaambia Mitume wao, «Lau Mwenyezi Mungu Angalitaka tumpwekeshe na tusiabudu chochote kisichokuwa Yeye, Angaliteremsha Malaika kutoka mbinguni wakiwa wajumbe wa hilo unalotuitia kwalo, na Hangaliwatuma nyinyi na hali nyinyui ni binadamu kama sisi, basi sisi kwa lile ambalo Mwenyezi Mungu Amewatuma kwetu la kumuamini Mwenyezi Mungu Peke Yake ni wenye kulikanusha.» info
التفاسير:

external-link copy
15 : 41

فَأَمَّا عَادٞ فَٱسۡتَكۡبَرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّ وَقَالُواْ مَنۡ أَشَدُّ مِنَّا قُوَّةًۖ أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّ ٱللَّهَ ٱلَّذِي خَلَقَهُمۡ هُوَ أَشَدُّ مِنۡهُمۡ قُوَّةٗۖ وَكَانُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَجۡحَدُونَ

Ama hao 'Ād, watu wa Hūd, waliwafanyia waja ujeuri bila haki na wakasema kwa kujiona, «Ni nani mwenye nguvu kali zaidi kushinda sisi?» Kwani hawaoni kuwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Aliyewaumba ni Mkali zaidi wa nguvu na kipigo? Na walikuwa ni wenye kuzikanusha hoja zeyu na dalili zetu. info
التفاسير:

external-link copy
16 : 41

فَأَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ رِيحٗا صَرۡصَرٗا فِيٓ أَيَّامٖ نَّحِسَاتٖ لِّنُذِيقَهُمۡ عَذَابَ ٱلۡخِزۡيِ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَخۡزَىٰۖ وَهُمۡ لَا يُنصَرُونَ

Tukawatumia wao upepo wenye ubaridi mkali, wenye sauti kubwa, katika siku zilizokuwa korofi, ili tuwaonjeshe adhabu ya unyonge na utwevu katika maisha ya kilimwengu. Na adhabu ya Akhera ina unyonge na utwevu mwingi zaidi, na wao hawatasaidiwa kwa kuzuia adhabu isiwapate. info
التفاسير:

external-link copy
17 : 41

وَأَمَّا ثَمُودُ فَهَدَيۡنَٰهُمۡ فَٱسۡتَحَبُّواْ ٱلۡعَمَىٰ عَلَى ٱلۡهُدَىٰ فَأَخَذَتۡهُمۡ صَٰعِقَةُ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡهُونِ بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Na ama hao Thamūd, watu wa Ṣāliḥ, kwa hakika tuliwabainishia njia ya uongofu na usawa, wakafadhilisha upofu juu ya uongofu, kikawaangamiza wao kimondo cha adhabu yenye kutweza kwa sababu ya dhambi waliokuwa wakizitenda kwa kumkufuru kwao Mwenyezi Mungu na kuwakanusha Mitume Wake. info
التفاسير:

external-link copy
18 : 41

وَنَجَّيۡنَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَكَانُواْ يَتَّقُونَ

Na tukawaokoa wale walioamini kutokana na adhabu iliyowapata kina 'Ād na Thamūd. Na hawa waliookoka walikuwa wanamuogopa Mwenyezi Mungu na kumcha. info
التفاسير:

external-link copy
19 : 41

وَيَوۡمَ يُحۡشَرُ أَعۡدَآءُ ٱللَّهِ إِلَى ٱلنَّارِ فَهُمۡ يُوزَعُونَ

Na Siku ambayo maadui wa Mwenyezi Mungu watakusanywa wapelekwe kwenye Moto wa Jahanamu, Malaika wa adhabu watawarudisha wa mwanzo wao wawakusanye na wa mwisho wao. info
التفاسير:

external-link copy
20 : 41

حَتَّىٰٓ إِذَا مَا جَآءُوهَا شَهِدَ عَلَيۡهِمۡ سَمۡعُهُمۡ وَأَبۡصَٰرُهُمۡ وَجُلُودُهُم بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

hata watakapoufikia Moto na wakakanusha makosa yao, yatatoa ushahidi dhidi yao masikio yao, macho yao na ngozi zao kwa yale ambayo walikuwa wakiyafanya duniani ya madhambi na makosa. info
التفاسير: