ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫

ߞߐߜߍ ߝߙߍߕߍ:close

external-link copy
80 : 16

وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّنۢ بُيُوتِكُمۡ سَكَنٗا وَجَعَلَ لَكُم مِّن جُلُودِ ٱلۡأَنۡعَٰمِ بُيُوتٗا تَسۡتَخِفُّونَهَا يَوۡمَ ظَعۡنِكُمۡ وَيَوۡمَ إِقَامَتِكُمۡ وَمِنۡ أَصۡوَافِهَا وَأَوۡبَارِهَا وَأَشۡعَارِهَآ أَثَٰثٗا وَمَتَٰعًا إِلَىٰ حِينٖ

Mwenyezi Mungu, Aliyetakata na sifa za upungufu, Amewapatia nyinyi mapumziko na utulivu kwenye nyumba zenu pamoja na watu wenu mkiwa mijini, na Amewapatia nyinyi mahema na mindule ya ngozi za wanyama- howa, ambayo ni sahali kwenu mkiwa safarini, na ambayo ni sahali kwenu kuisimamisha pale mkaapo baada ya safari, na Amewapatia nyinyi kutokana na manyoya ya kondoo, manywele ya ngamia na nwyele za mbuzi vyombo vya matumizi yenu ya kuvaa, kujifinika, kutandika na pambo la nyinyi kujifurahisha kwalo mpaka kipindi kilichotajwa na wakati ujulikanao. info
التفاسير:

external-link copy
81 : 16

وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّمَّا خَلَقَ ظِلَٰلٗا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ ٱلۡجِبَالِ أَكۡنَٰنٗا وَجَعَلَ لَكُمۡ سَرَٰبِيلَ تَقِيكُمُ ٱلۡحَرَّ وَسَرَٰبِيلَ تَقِيكُم بَأۡسَكُمۡۚ كَذَٰلِكَ يُتِمُّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تُسۡلِمُونَ

Na Mwenyezi Mungu Amewaptia miti na vinginevyo vya kuwaletea vivuli, na amewafanyia kwenye majabali na pango sehemu za kuhamia mnapohitajia, na Amewafanyia nguo kutokana na pamba na sufi na vinginevyo za kuwahifadhi na joto na baridi, na Amewaumbia chuma cha nyinyi kujikinga na silaha za kudunga za maadui wenu na madhara yao katika vita vyenu na wao. Kama vile Alivyowaneemesha kwa neema hizi, atawakamilishia neema Zake kwenu kwa kuwafafanulia wazi Dini ya haki, ili mjisalimishe kwa amri ya Mwenyezi Mungu, Peke Yake, na msimshirikishe na kitu chochote katika ibada Yake. info
التفاسير:

external-link copy
82 : 16

فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Wakikupa mgongo, ewe Mtume, baada ya kuziona hizi aya, basi usisikitike. Kwani jukumu lako ni kuufikisha ujumbe uliotumwa nao waziwazi, ama kuongoa ni kwetu sisi. info
التفاسير:

external-link copy
83 : 16

يَعۡرِفُونَ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ ثُمَّ يُنكِرُونَهَا وَأَكۡثَرُهُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ

Washirikina hawa wazijua neema za Mwenyezi Mungu juu yao za kutumilizwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwao, kisha wanaukanusha utume wake. Na wengi wa watu wake ni wale wanaoukanusha utume wake na sio wanaoukubali. info
التفاسير:

external-link copy
84 : 16

وَيَوۡمَ نَبۡعَثُ مِن كُلِّ أُمَّةٖ شَهِيدٗا ثُمَّ لَا يُؤۡذَنُ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ وَلَا هُمۡ يُسۡتَعۡتَبُونَ

Na wakumbushe, ewe Mtume, yale yatakayokuwa Siku ya Kiyama, tutakapowaletea kila kundi la watu Mtume wao akitolea ushahidi Imani ya walioamini miongoni mwao na ukanushaji wa wenye kukanusha. Kisha hao waliokanusha hawatapewa nafasi ya kuomba msamaha kwa waliyoyafanya, na hawatatakiwa kumridhisha Mola wao kwa kutubia na kufanya matendo mema, kwani wakati wa hilo ushapita. info
التفاسير:

external-link copy
85 : 16

وَإِذَا رَءَا ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ ٱلۡعَذَابَ فَلَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمۡ وَلَا هُمۡ يُنظَرُونَ

Na wale waliokanusha watakapoishuhudia adhabu ya Mwenyezi huko Akhera, basi hawatapunguziwa chochote katika hiyo adhabu, hawatapewa muhula wala hawatacheleweshwa. info
التفاسير:

external-link copy
86 : 16

وَإِذَا رَءَا ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْ شُرَكَآءَهُمۡ قَالُواْ رَبَّنَا هَٰٓؤُلَآءِ شُرَكَآؤُنَا ٱلَّذِينَ كُنَّا نَدۡعُواْ مِن دُونِكَۖ فَأَلۡقَوۡاْ إِلَيۡهِمُ ٱلۡقَوۡلَ إِنَّكُمۡ لَكَٰذِبُونَ

Na wale waliokanusha watakapowaona Siku ya Kiyama waungu wao waliokuwa wakiwaabudu pamoja na MwenyeziMungu watasema, «Mola wetu! Hawa ndio washirika wetu tuliokuwa tukiwaabudu badala yako.» Hapo waungu hao watatamka kuwakanusha wale waliowaabudu na watasema, «Hakika nyinyi, enyi washirikina, ni warongo, mlipotufanya sisi ni washirika wa Mwenyezi Mungu na mkatuabudu pamoja na Yeye. Sisi hatukuwaamuru hilo, wala hatukudai kwamba sisi tunastahiki uungu, lawama ni juu yenu.» info
التفاسير:

external-link copy
87 : 16

وَأَلۡقَوۡاْ إِلَى ٱللَّهِ يَوۡمَئِذٍ ٱلسَّلَمَۖ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Na hiyo Siku ya Kiyama, washirikina wataonyesha kusalimu amri na unyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu, na yatawapotea yale ya urongo waliokuwa wakiyazua na kwamba waungu wao watawaombea. info
التفاسير: