पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - स्वाहिली अनुवाद : अली मुहसिन बरवानी ।

رقم الصفحة:close

external-link copy
77 : 56

إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ

Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu, info

Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani yenye manufaa mengi,

التفاسير:

external-link copy
78 : 56

فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ

Katika Kitabu kilicho hifadhiwa. info

Imo katika ubao ulio hifadhiwa Al-lauhu-lmahfudh, usio karibiwa na yeyote ila Malaika walio karibishwa kwa Mwenyezi Mungu. (Kwa watumiaji Computer wanaweza kukisia kuwa hiyo Al-lauhu-lmahfudh ni kama Disk iliyomo ndani ya Computer na haigusi mtu, na Misahafu tunayo iona, na kuisoma, ni kama yapigwayo chapa kutoka hiyo Disk.)

التفاسير:

external-link copy
79 : 56

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ

Hapana akigusaye ila walio takaswa. info

Hawaigusi Qur'ani Tukufu ila walio t'ahirika na najisi na hadathi, vitengua udhu;

التفاسير:

external-link copy
80 : 56

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. info

imeteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa viumbe vyote.

التفاسير:

external-link copy
81 : 56

أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ

Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza? info

Je! Mnapuuza? Ni Qur'ani hii tukufu ndio nyinyi mnaidharau?

التفاسير:

external-link copy
82 : 56

وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha? info

Na badala ya kuishukuru riziki yenu ndio mna ikadhibisha?

التفاسير:

external-link copy
83 : 56

فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ

Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo, info

Basi je! Ikifika roho ya mmoja wenu kwenye mapitio ya pumzi,

التفاسير:

external-link copy
84 : 56

وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ

Na nyinyi wakati huo mnatazama! info

Na nyinyi inapo fika roho kwenye koo nanyi mnamwangalia huyo anaye kufa,

التفاسير:

external-link copy
85 : 56

وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ

Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi. info

Na Sisi tuko karibu zaidi kwa huyo aliye kabiliwa na mauti na tunaijua zaidi hali yake kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamjui hayo wala hamhisi.

التفاسير:

external-link copy
86 : 56

فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ

Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu, info

Basi je! Ikiwa nyinyi si wenye kunyenyekea kwa Ungu wetu,

التفاسير:

external-link copy
87 : 56

تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli? info

Mrudishieni roho yake huyo aliye kabiliwa na mauti ikiwa nyinyi mwasema kweli kwamba nyinyi mnazo nguvu na hamshindwi.

التفاسير:

external-link copy
88 : 56

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa, info

Ama akiwa huyo aliye kabiliwa na mauti ni katika walio tangulia walio karibishwa ,

التفاسير:

external-link copy
89 : 56

فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema. info

Basi mwisho wake ni raha, na rehema, na riziki njema, na Pepo yenye neema.

التفاسير:

external-link copy
90 : 56

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Na akiwa katika watu wa upande wa kulia, info

Ama akiwa katika watu wa mkono wa kulia,

التفاسير:

external-link copy
91 : 56

فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia. info

Basi ataambiwa kwa maamkio na takrima: Unapewa salamu kutokana na watu wa kuliani.

التفاسير:

external-link copy
92 : 56

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ

Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu, info

Na ama akiwa ni katika wa kushoto, wanao kanusha, walio wapotovu,

التفاسير:

external-link copy
93 : 56

فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ

Basi karamu yake ni maji yanayo chemka, info

Basi atakirimiwa maji ya moto hadi ya kuchemka,

التفاسير:

external-link copy
94 : 56

وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ

Na kutiwa Motoni. info

Na kubabuliwa na moto wa mwisho wa ukali.

التفاسير:

external-link copy
95 : 56

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ

Hakika hii ndiyo haki yenye yakini. info

Hakika haya yaliyo tajwa katika Sura hii tukufu bila ya shaka ni kiini cha yakini iliyo thibiti, isiyo ingiliwa na shaka.

التفاسير:

external-link copy
96 : 56

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa. info

Tanguliza tasbihi kwa kumdhukuru Mola wako Mlezi aliye Mkubwa, kwa kumtakasa na kumshukuru kwa neema zake.

التفاسير: