पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - स्वाहिली अनुवाद : अली मुहसिन बरवानी ।

رقم الصفحة:close

external-link copy
6 : 11

۞ وَمَا مِن دَآبَّةٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ إِلَّا عَلَى ٱللَّهِ رِزۡقُهَا وَيَعۡلَمُ مُسۡتَقَرَّهَا وَمُسۡتَوۡدَعَهَاۚ كُلّٞ فِي كِتَٰبٖ مُّبِينٖ

NA HAKUNA mnyama yoyote katika ardhi ila riziki yake iko kwa Mwenyezi Mungu. Naye anajua makao yake na mapitio yake. Yote yamo katika Kitabu chenye kubainisha. info

Na wajue watu hawa kuwa uwezo wa Mwenyezi Mungu na neema zake, na ujuzi wake, umeenea kila kitu. Basi hapana mnyama anaye furukuta katika ardhi ila Mwenyezi Mungu kwa fadhila yake kesha mtengenezea riziki yake inayo wafikiana naye katika hali mbali mbali. Naye anajua anakaa wapi katika hali ya uhai wake, na pahala atapo wekwa wakati wa kufa kwake! Kila kitu katika hayo kimekwisha dhibitiwa kwake Subhanahu katika Kitabu chenye kuweka wazi hali zote ziliomo.

التفاسير:

external-link copy
7 : 11

وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ وَكَانَ عَرۡشُهُۥ عَلَى ٱلۡمَآءِ لِيَبۡلُوَكُمۡ أَيُّكُمۡ أَحۡسَنُ عَمَلٗاۗ وَلَئِن قُلۡتَ إِنَّكُم مَّبۡعُوثُونَ مِنۢ بَعۡدِ ٱلۡمَوۡتِ لَيَقُولَنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٞ

Na Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Na Kiti chake cha Enzi kilikuwa juu ya maji, ili akufanyieni mtihani ajuulikane ni nani miongoni mwenu mzuri zaidi wa vitendo. Na wewe ukisema: Nyinyi hakika mtafufuliwa baada ya kufa; wale walio kufuru husema: Hayakuwa haya ila ni uchawi uliyo wazi. info

Na Mwenyezi Mungu kaziumba mbingu na ardhi na viliomo ndani yake katika siku sita. Na kabla ya hapo palikuwa hapana chochote zaidi kuliko ulimwengu wa maji, na juu yake A'rshi, Kiti cha Enzi cha Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ameumba ulimwengu wote huu ili adhihirishe kwa kukujaribuni hali zenu, enyi watu, atokeze kati yenu anaye mkubali Mwenyezi Mungu kwa ut'iifu na vitendo vyema, na nani anaye yaacha hayo...Na juu ya uwezo huu wa kuumba, ukiwaambia kwa yakini: Nyinyi mtafufuliwa kutoka makaburini kwenu, na kwamba wao wameumbwa ili wafe na wafufuliwe, wao mbio mbio wanakurudi kwa mkazo kuwa haya mliyo kuja nayo hayana ukweli wowote! Wala hayo si chochote ila ni kama uchawi ulio wazi wa kuchezea akili tu.

التفاسير:

external-link copy
8 : 11

وَلَئِنۡ أَخَّرۡنَا عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابَ إِلَىٰٓ أُمَّةٖ مَّعۡدُودَةٖ لَّيَقُولُنَّ مَا يَحۡبِسُهُۥٓۗ أَلَا يَوۡمَ يَأۡتِيهِمۡ لَيۡسَ مَصۡرُوفًا عَنۡهُمۡ وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Na tukiwacheleweshea adhabu mpaka muda ulio kwisha hisabiwa wao husema: Nini kinacho izuia hiyo adhabu? Jueni! Siku itakapo wajia basi haitoondolewa hiyo kwao. Na yatawazunguka yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha. info

Ilivyo kuwa hikima yetu ni kuakhirisha adhabu ya ukafiri wao hapa duniani mpaka wakati tuliyo uweka, nao ni Siku ya Kiyama, wao husema kwa kejeli: Nini kinacho mzuia hivi sasa? Na ailete hiyo adhabu ikiwa anasema kweli katika hiyo ahadi yake! Basi nawajue hao kwamba adhabu itakuja tu bila ya muhali. Na itapo wajia hawatapata kuokoka, na itawazunguka kwa sababu ya kejeli zao na kutaka kuvunja hishima.

التفاسير:

external-link copy
9 : 11

وَلَئِنۡ أَذَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِنَّا رَحۡمَةٗ ثُمَّ نَزَعۡنَٰهَا مِنۡهُ إِنَّهُۥ لَيَـُٔوسٞ كَفُورٞ

Na tukimwonjesha mtu rehema inayo toka kwetu, kisha tukamwondolea, hukata tamaa akakufuru. info

Na katika tabia za binaadamu ni kujizamisha mwenyewe katika hali aliyo nayo. Basi tukimpa baadhi ya neema na rehema, kama vile afya nzuri, na ukunjufu wa riziki, kisha baadae tukamwondolea neema hizo, kwa mujibu wa mipango yetu, yeye hupita mipaka katika kukata tamaa kuwa neema hiyo haitorudi tena; na akapita mipaka katika kuzikufuru neema nyengine ambazo bado angali anastarehe nazo.

التفاسير:

external-link copy
10 : 11

وَلَئِنۡ أَذَقۡنَٰهُ نَعۡمَآءَ بَعۡدَ ضَرَّآءَ مَسَّتۡهُ لَيَقُولَنَّ ذَهَبَ ٱلسَّيِّـَٔاتُ عَنِّيٓۚ إِنَّهُۥ لَفَرِحٞ فَخُورٌ

Na tukimwonjesha neema baada ya madhara yaliyo mpata husema: Taabu zimekwisha niondokea. Hakika yeye hujitapa na kutafakhari. info

Na tukimpa neema baada ya shida aliyo kuwa nayo yeye husema: Shida zangu zote zimekwisha niondokea, wala hazitarudi tena! Na hayo humpelekea upeo wa kufurahikia starehe za dunia, na kujifakhirisha bila ya kiasi. Moyo wake huwa umeshughulika, usimshukuru Mola wake Mlezi! Hii ndiyo hali ya binaadamu wengi, wanababaika baina ya kukata tamaa na kujitapa!

التفاسير:

external-link copy
11 : 11

إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ أُوْلَٰٓئِكَ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَأَجۡرٞ كَبِيرٞ

Ila wale walio subiri wakatenda mema. Hao watapata msamaha na ujira mkubwa. info

Na aibu hii hawaachi kuwa nayo ila wale wanao subiri wakati wa dhiki, na wakatenda mema wakati wa faraji na shida. Hawa watasamehewa dhambi zao, na watapata ujira mkubwa kwa vitendo vyao vyema.

التفاسير:

external-link copy
12 : 11

فَلَعَلَّكَ تَارِكُۢ بَعۡضَ مَا يُوحَىٰٓ إِلَيۡكَ وَضَآئِقُۢ بِهِۦ صَدۡرُكَ أَن يَقُولُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ كَنزٌ أَوۡ جَآءَ مَعَهُۥ مَلَكٌۚ إِنَّمَآ أَنتَ نَذِيرٞۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٌ

Basi labda utaacha baadhi ya yale yaliyo funuliwa kwako, na kifua kitaona dhiki kwa hayo, kwa sababu wanasema: Mbona hakuteremshiwa khazina, au wakaja naye Malaika? Wewe ni mwonyaji tu, na Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wa kila kitu. info

Ewe Nabii! Usijaribu kutaka kuwaridhi washirikina, kwani hao hawaamini. Na huenda ukijaribu kutaka kuwaridhi ukaacha kusoma baadhi ya uliyo letewa Wahyi, katika yale wasiyo penda wao kuyasikia, kama vile kudharauliwa baadhi ya miungu yao, kwa kukhofu kuwa wasije wakakejeli! Na huenda pengine ukahisi dhiki unapo wasomea, kwa kuwa wao wanataka Mwenyezi Mungu akuteremshie khazina ustarehe nayo kama wafalme, au waje nawe malaika watwambie ukweli wake! Basi, ewe Nabii! Usizibali inadi zao. Kwani wewe si chochote ila ni mwonyaji na mhadharishaji wa adhabu za Mwenyezi Mungu kwa anaye kwenda kinyume na amri yake. Nawe hayo umefanya, basi jipumzishe nafsi yako nao. Na jua kuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuangalia na kulinda kila kitu. Naye atawafanyia kama wanavyo stahiki.

التفاسير: