വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്.

പേജ് നമ്പർ:close

external-link copy
155 : 4

فَبِمَا نَقۡضِهِم مِّيثَٰقَهُمۡ وَكُفۡرِهِم بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَقَتۡلِهِمُ ٱلۡأَنۢبِيَآءَ بِغَيۡرِ حَقّٖ وَقَوۡلِهِمۡ قُلُوبُنَا غُلۡفُۢۚ بَلۡ طَبَعَ ٱللَّهُ عَلَيۡهَا بِكُفۡرِهِمۡ فَلَا يُؤۡمِنُونَ إِلَّا قَلِيلٗا

Tukawalaani kwa sababu ya kuvunja kwao ahadi, kukanusha kwao aya za Mwenyezi Mungu zinazojulisha ukweli wa Mitume Wake, kuua kwao Manabii wa Mwenyezi Mungu kwa maonevu na uadui na kwa kusema kwao, «Nyoyo zetu zimezibwa kwa vifiniko, hatuyafahamu uyasemayo.» Bali Mwenyezi Mungu ameziziba kwa sababu ya ukafiri wao. Kwa hivyo, hawataamini isipokuwa Imani isiyowafaa. info
التفاسير:

external-link copy
156 : 4

وَبِكُفۡرِهِمۡ وَقَوۡلِهِمۡ عَلَىٰ مَرۡيَمَ بُهۡتَٰنًا عَظِيمٗا

Na vile vile tuliwalaani kwa sababu ya ukafiri wao na kumzulia kwao Maryam urongo kwa yale waliyomsingizia nayo ya uzinifu na hali yeye yupo mabali na hilo. info
التفاسير:

external-link copy
157 : 4

وَقَوۡلِهِمۡ إِنَّا قَتَلۡنَا ٱلۡمَسِيحَ عِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ رَسُولَ ٱللَّهِ وَمَا قَتَلُوهُ وَمَا صَلَبُوهُ وَلَٰكِن شُبِّهَ لَهُمۡۚ وَإِنَّ ٱلَّذِينَ ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ لَفِي شَكّٖ مِّنۡهُۚ مَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍ إِلَّا ٱتِّبَاعَ ٱلظَّنِّۚ وَمَا قَتَلُوهُ يَقِينَۢا

Na- pia tuliwalaani- kwa sababu ya neno lao, kwa njia ya kukejeli na shere, «Sisi tumemuua Al- Masīh,, ‘Īsā mwana wa Maryam, mjumbe wa Mwenyezi Mungu.» Na wala wao hawakumuua ‘Īsā wala hawakumsulubu, bali walimsulubu mwanamume aliyefanana naye kwa kudhani kwao kuwa yeye ndiye ‘Īsā. Na yoyote aliyedai kwamba walimuua, miongoni mwa Mayahudi na pia wale waliomsalimisha kwao, miongoni mwaWanaswara, wote hao wako kwenye shaka na kuchanganyikiwa; hawana ujuzi wowote isipokua ni kufuata dhana tu, na wala hawana yakini ya kuwa walimuua, bali wana shaka nalo hilo na wanalidhania tu. info
التفاسير:

external-link copy
158 : 4

بَل رَّفَعَهُ ٱللَّهُ إِلَيۡهِۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَزِيزًا حَكِيمٗا

Bali Mwenyezi Mungu Alimpaisha ‘Īsā kwa mwili wake na roho yake akiwa hai na Alimuokoa na wale waliokufuru. Na Mwenyezi Mungu ni Mshindi katika ufalme Wake, ni Mwingi wa hekima katika uendeshaji mambo Wake na mapitisho Yake. info
التفاسير:

external-link copy
159 : 4

وَإِن مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ إِلَّا لَيُؤۡمِنَنَّ بِهِۦ قَبۡلَ مَوۡتِهِۦۖ وَيَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يَكُونُ عَلَيۡهِمۡ شَهِيدٗا

Na kwa hakika hatasalia yoyote, kati ya wale waliopewa Kitabu, baada ya kuteremka ‘Īsā zama za mwisho, isipokuwa atamuamini Nabii ‘Īsā kabla ya kufa kwake, amani imshukie, na siku ya Kiyama Nabii ‘Īsā atakuwa ni shahidi kwamba waliomkanusha walikuwa warongo na waliomuamini walikuwa wakweli. info
التفاسير:

external-link copy
160 : 4

فَبِظُلۡمٖ مِّنَ ٱلَّذِينَ هَادُواْ حَرَّمۡنَا عَلَيۡهِمۡ طَيِّبَٰتٍ أُحِلَّتۡ لَهُمۡ وَبِصَدِّهِمۡ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ كَثِيرٗا

Na kwa sababu ya dhuluma ya Mayahudi kwa madhambi makubwa waliyoyafanya, Mwenyezi Mungu Aliwaharamishia vyakula vizuri vilivyokuwa halali kwao, na pia kwa sababu ya kuzizuia nafsi zao na kuwazuia wengine wao wasiifuate dini ya Mwenyezi Mungu iliyo ya sawa. info
التفاسير:

external-link copy
161 : 4

وَأَخۡذِهِمُ ٱلرِّبَوٰاْ وَقَدۡ نُهُواْ عَنۡهُ وَأَكۡلِهِمۡ أَمۡوَٰلَ ٱلنَّاسِ بِٱلۡبَٰطِلِۚ وَأَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ مِنۡهُمۡ عَذَابًا أَلِيمٗا

Na kwa sababu ya kutumia kwao riba ambayo walikatazwa wasitumie na kujihalalishia kwao mali za watu pasi na haki. Na tumewatayarishia waliomkanusha Mwenyezi Mungu na Mtume Wake adhabu iumizayo huko Akhera. info
التفاسير:

external-link copy
162 : 4

لَّٰكِنِ ٱلرَّٰسِخُونَ فِي ٱلۡعِلۡمِ مِنۡهُمۡ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ يُؤۡمِنُونَ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ وَمَآ أُنزِلَ مِن قَبۡلِكَۚ وَٱلۡمُقِيمِينَ ٱلصَّلَوٰةَۚ وَٱلۡمُؤۡتُونَ ٱلزَّكَوٰةَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ أُوْلَٰٓئِكَ سَنُؤۡتِيهِمۡ أَجۡرًا عَظِيمًا

Lakini wale waliojikita katika elimu katika hukumu za Mwenyezi Mungu kati ya Mayahudi na wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, wanayaamini yale Aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu kwako, ewe Mtume, nayo ni Qur’ani, na yale Aliyoyateremsha kwa Mitume kabla yako, kama Taurati na Injili, wanatekeleza Swala kwa nyakati zake, wanatoa Zaka za mali zao na wanamuamini Mwenyezi Mungu, kufufuliwa na malipo. Hao Mwenyezi Mungu Atawapa thawabu kubwa, nayo ni Pepo. info
التفاسير: