വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്.

external-link copy
67 : 2

وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِۦٓ إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُكُمۡ أَن تَذۡبَحُواْ بَقَرَةٗۖ قَالُوٓاْ أَتَتَّخِذُنَا هُزُوٗاۖ قَالَ أَعُوذُ بِٱللَّهِ أَنۡ أَكُونَ مِنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ

Na Kumbukeni, enyi wana wa Isrāīl, makosa ya mababu zenu, ushindani wao mwingi na kujadiliana kwao na Mūsā, rehema na amani zimshukie, pindi alipowaambia, “Hakika Mwenyezi Mungu Anawaamuru mchinje ng’ombe.” Wakasema, wakiwa na kiburi, “Unatufanyia mzaha na kutuchezea?” Mūsā akawajibu, “Ninajilinda kwa Mwenyezi Mungu nisiwe ni miongoni mwa wanaofanya stihizai.” info
التفاسير: