വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്.

An-Nahl

external-link copy
1 : 16

أَتَىٰٓ أَمۡرُ ٱللَّهِ فَلَا تَسۡتَعۡجِلُوهُۚ سُبۡحَٰنَهُۥ وَتَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Kumekaribia kusimama Kiyama na kutoka amri ya Mwenyezi Mungu ya kuwaadhibu nyinyi, enyi makafiri, basi msiifanyie haraka adhabu kwa njia ya kuicheza shere ahadi ya Mtume kwenu. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ameepukana na ushirika na washirikina. info
التفاسير:

external-link copy
2 : 16

يُنَزِّلُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ بِٱلرُّوحِ مِنۡ أَمۡرِهِۦ عَلَىٰ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦٓ أَنۡ أَنذِرُوٓاْ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱتَّقُونِ

Mwenyezi Mungu Anawateremsha Malaika kuleta wahyi kwa amri Yake kwa anayemtaka miongoni mwa waja Wake waliotumilizwa kwamba watisheni watu na ushirikina na waambieni kwamba hapana wa kuabudiwa kwa haki isipokuwa mimi. Hivyo basi, nicheni kwa kutekeleza faradhi zangu na kunipwekesha kwa kuniabudu na kunitakasa. info
التفاسير:

external-link copy
3 : 16

خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۚ تَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Ameziumba mbingu na ardhi kwa haki, ili waja kwa hizo wachukue ushahidi juu ya utukufu wa Muumba wa hizo na kwamba, Yeye Peke Yake, Ndiye Anayestahiki kuabudiwa, Ameepukana, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, na Ametukuka na ushirikina wao. info
التفاسير:

external-link copy
4 : 16

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٖ فَإِذَا هُوَ خَصِيمٞ مُّبِينٞ

Amemuumba binadamu kutokana na maji matwevu, akitahamaki ajiona ana nguvu na majivuno, na akawa mkali wa utesi na kumjadili Mola wake katika kukanusha kufufuliwa na mengineyo, kama vile kusema, «Ni nani atakayeihuisha mifupa iwapo imeoza.» Na akawa ni mwenye kumsahau Mwenyezi Mungu Aliyemuumba kutoka kwenye hali ya kutokuwako. info
التفاسير:

external-link copy
5 : 16

وَٱلۡأَنۡعَٰمَ خَلَقَهَاۖ لَكُمۡ فِيهَا دِفۡءٞ وَمَنَٰفِعُ وَمِنۡهَا تَأۡكُلُونَ

Na wanyama miongoni mwa ngamia, ng’ombe na mbuzi, Mwenyezi Mungu Amewaumbia, enyi watu, na akajaalia joto katika sufi na manyoa yake, na manufaa mengine katika maziwa yake na ngozi zake na kuwatumia kwa kuwapanda na, wengine miongoni mwao, kuwala. info
التفاسير:

external-link copy
6 : 16

وَلَكُمۡ فِيهَا جَمَالٌ حِينَ تُرِيحُونَ وَحِينَ تَسۡرَحُونَ

Na muna, kwa wanyama hao, pambo linaloingiza furaha kwenu, pindi mnapowarudisha kwenye mazizi yao jioni na pindi mnapowatoa kukicha kuwapeleka malishoni. info
التفاسير: