വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്.

പേജ് നമ്പർ:close

external-link copy
43 : 14

مُهۡطِعِينَ مُقۡنِعِي رُءُوسِهِمۡ لَا يَرۡتَدُّ إِلَيۡهِمۡ طَرۡفُهُمۡۖ وَأَفۡـِٔدَتُهُمۡ هَوَآءٞ

Siku watakaosimama madhalimu kutoka makaburini mwao wakikimbilia kumwitika mlinganizi wakiinua vichwa vyao, hawaoni chote kwa kituko cha kisimamo, na hali nyoyo zao ni tupu hazina kitu ndani yake, kwa kicho kingi na kuogopa ktuko cha wanayoyaona. info
التفاسير:

external-link copy
44 : 14

وَأَنذِرِ ٱلنَّاسَ يَوۡمَ يَأۡتِيهِمُ ٱلۡعَذَابُ فَيَقُولُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ رَبَّنَآ أَخِّرۡنَآ إِلَىٰٓ أَجَلٖ قَرِيبٖ نُّجِبۡ دَعۡوَتَكَ وَنَتَّبِعِ ٱلرُّسُلَۗ أَوَلَمۡ تَكُونُوٓاْ أَقۡسَمۡتُم مِّن قَبۡلُ مَا لَكُم مِّن زَوَالٖ

Na waonye, ewe Mtume, wale watu ambao wewe umetumilizwa kwao, adhabu ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama. Na hapo wale waliojidhulumu kwa kukanusha watasema, «Ewe Mola,wetu! Tupe muhula wa muda mchache, tutakuamini na tutawasadiki Mitume wako. Na wataambiwa kwa kujereshwa, «Je, hamkuapa katika uhai wenu kwamba hamtaondoka ulimwenguni kwenda Akhera, na msiamini kufufuliwa huku? info
التفاسير:

external-link copy
45 : 14

وَسَكَنتُمۡ فِي مَسَٰكِنِ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ وَتَبَيَّنَ لَكُمۡ كَيۡفَ فَعَلۡنَا بِهِمۡ وَضَرَبۡنَا لَكُمُ ٱلۡأَمۡثَالَ

«Na mkakaa kwenye makao ya makafiri waliopita waliojidhulumu nafsi zao, kama vile watu wa Hūd na Ṣāliḥ, na mkajua, kwa mlivyoona na mlivyombiwa, maangamivu tuliyowateremshia na tukawapigia mifano katika Qur’ani msizingatie?» info
التفاسير:

external-link copy
46 : 14

وَقَدۡ مَكَرُواْ مَكۡرَهُمۡ وَعِندَ ٱللَّهِ مَكۡرُهُمۡ وَإِن كَانَ مَكۡرُهُمۡ لِتَزُولَ مِنۡهُ ٱلۡجِبَالُ

Na kwa kweli, washirikina walimpangia njama Mtume, rehema na amani zimshukie, za kumuua. Na vitimbi vyao vilikuwako kwa Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Yeye Amewazunguka. Na vitimbi vyao vikawarudia wenyewe. Na havikuwa vitimbi vyao ni vyenye kuondoa majabali wala vitu vinginevyo kwa udhaifu wake na unyonge wake. Na wao hawakumdhuru Mwenyezi Mungu, lakini walijidhuru wenyewe. info
التفاسير:

external-link copy
47 : 14

فَلَا تَحۡسَبَنَّ ٱللَّهَ مُخۡلِفَ وَعۡدِهِۦ رُسُلَهُۥٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٞ ذُو ٱنتِقَامٖ

Basi usidhanie, ewe Mtume, kwamba Mwenyezi Mungu Atakwenda kinyume na vile Alivyowaahidi Mitume Wake, kuwa Atawapa ushindi na Atawaangamiza wenye kuwakanusha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mshindi, hakuna kitu kinachomshinda kukifanya, ni Mwenye kuwalipiza maadui wake kwa kuwapa mateso makali kabisa. Maneno haya ingawa anaambiwa Nabii, rehema na amani zimshukie, yanaelekezwa kwa ummah wote. info
التفاسير:

external-link copy
48 : 14

يَوۡمَ تُبَدَّلُ ٱلۡأَرۡضُ غَيۡرَ ٱلۡأَرۡضِ وَٱلسَّمَٰوَٰتُۖ وَبَرَزُواْ لِلَّهِ ٱلۡوَٰحِدِ ٱلۡقَهَّارِ

Na malipizo ya Mwenyezi Mungu ya kuwatesa maadui Wake Siku ya Kiyama yatakuwa kwenye siku ambayo itabadilishwa hii ardhi kwa ardhi nyingine nyeupe iliyotakata kama fedha, na vilevile zitatabadilishwa mbingu kwa nyingine, na watatoka viumbe makaburini mwao wakiwa hai wakiwa wamejitokeza kukutana na Mwenyezi Mungu Aliye Mmoja, Mwenye kutendesha nguvu, Aliyepwekeka kwa utukufu Wake, majina Yake, sifa Zake na matendo Yake na kulazimisha Kwake kila kitu. info
التفاسير:

external-link copy
49 : 14

وَتَرَى ٱلۡمُجۡرِمِينَ يَوۡمَئِذٖ مُّقَرَّنِينَ فِي ٱلۡأَصۡفَادِ

Na utawaona,ewe Nabii, waasi Siku ya Kiyama wamefungwa pingu, mikono yao miguu yao yamekutanishwa pamoja kwa minyonyoro, na hali wakiwa watwevu. info
التفاسير:

external-link copy
50 : 14

سَرَابِيلُهُم مِّن قَطِرَانٖ وَتَغۡشَىٰ وُجُوهَهُمُ ٱلنَّارُ

Nguo zao ni za rojo la mafuta linalochomeka sana, na hapo moto utaziramba nyuso zao na kuzichoma. info
التفاسير:

external-link copy
51 : 14

لِيَجۡزِيَ ٱللَّهُ كُلَّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Mwenyezi Mungu Atawafanyia hayo yakiwa ni malipo yao kwa madhambi waliyoyachuma duniani. Na Mwenyezi Mungu Atamlipa kila binadamu kwa alilolitenda, baya au zuri. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mpesi wa kuhesabu. info
التفاسير:

external-link copy
52 : 14

هَٰذَا بَلَٰغٞ لِّلنَّاسِ وَلِيُنذَرُواْ بِهِۦ وَلِيَعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا هُوَ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ وَلِيَذَّكَّرَ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Hii Qur’ani tuliyokuteremshia, ewe Mtume, ni maelezo na ni tangazo kwa watu, kwa kuwashauri na kuwatisha, na ili wawe na yakini kwamba Mwenyezi Mungu ni Mola Mmoja, wapate kumuabudu, Peke Yake, Asiye na Mshirika, na wapate kuwaidhika kwayo wenye akili timamu. info
التفاسير: