വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്.

പേജ് നമ്പർ:close

external-link copy
6 : 13

وَيَسۡتَعۡجِلُونَكَ بِٱلسَّيِّئَةِ قَبۡلَ ٱلۡحَسَنَةِ وَقَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِهِمُ ٱلۡمَثُلَٰتُۗ وَإِنَّ رَبَّكَ لَذُو مَغۡفِرَةٖ لِّلنَّاسِ عَلَىٰ ظُلۡمِهِمۡۖ وَإِنَّ رَبَّكَ لَشَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Na wale wakanushaji wanakuharakisha uwaletee adhabu ambayo mimi sikuwaharakishia kabla ya kuamini Imani ambayo kwayo kunatarajiwa usalama na matendo mema. Na yashapita mateso ya wakanushaji kabla yao, kwa nini wao hawawi ni wenye kuwaidhika na wao? Hakika Mola wako ni Mwenye msamaha wa dhambi za watu waliotubia dhambi zao juu ya udhalimu wao, Atawafungulia mlango wa msamaha na Atawaita waingie, na huku wao wanazidhulumu nafsi zao kwa kumuasi Mola wao. Hakika Mola Wako ni Mkali wa mateso juu ya walioendelea kwenye ukafiri, upotevu na kumuasi Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
7 : 13

وَيَقُولُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ ءَايَةٞ مِّن رَّبِّهِۦٓۗ إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرٞۖ وَلِكُلِّ قَوۡمٍ هَادٍ

Na makafiri wa Makkah wanasema, «Basi si ajiwe na miujiza inayoonekana kama fimbo ya Mūsā na ngamia wa Ṣāliḥ.» Na hilo haliko kwenye mkono wako, ewe Mtume; hukuwa wewe isipokuwa ni mwenye kuwafikishia na ni mwenye kuwatisha adhabu ya Mwenyezi Mungu. Na kila ummah una mjumbe wa kuwaongoza kwenye njia ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. info
التفاسير:

external-link copy
8 : 13

ٱللَّهُ يَعۡلَمُ مَا تَحۡمِلُ كُلُّ أُنثَىٰ وَمَا تَغِيضُ ٱلۡأَرۡحَامُ وَمَا تَزۡدَادُۚ وَكُلُّ شَيۡءٍ عِندَهُۥ بِمِقۡدَارٍ

Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Anakijua alichokibeba kila mwanamke ndani ya tumbo lake: ni cha kiume au ni cha kike, ni chema au ni kibaya. Na anakijua kile ambacho zao zinakipunguza kikazaliwa kimekufa au kabla ya kutimia myezi tisa au kikapita muda huo. Na kila kitu, chenye kuzidi au kupungua, kimekadiriwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa kipimo kisichopitisha kiasi. info
التفاسير:

external-link copy
9 : 13

عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِ ٱلۡكَبِيرُ ٱلۡمُتَعَالِ

Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyofichika na macho na yanayoonekana, Aliye Mkubwa wa dhati, majina na sifa , Aliye juu ya viumbe Vyake vyote kwa dhati Yake, uweza Wake na kutendesha nguvu Kwake. info
التفاسير:

external-link copy
10 : 13

سَوَآءٞ مِّنكُم مَّنۡ أَسَرَّ ٱلۡقَوۡلَ وَمَن جَهَرَ بِهِۦ وَمَنۡ هُوَ مُسۡتَخۡفِۭ بِٱلَّيۡلِ وَسَارِبُۢ بِٱلنَّهَارِ

Analingana, katika ujuzi Wake Aliyetukuka, yule anayesirisha maneno, katika nyinyi, na anayedhihirisha. Na analingana Kwake yule anayefanya matendo yake kwa siri ndani ya giza la usiku na yule mwenye kuyafanya waziwazi kwenye mwangaza wa mchana. info
التفاسير:

external-link copy
11 : 13

لَهُۥ مُعَقِّبَٰتٞ مِّنۢ بَيۡنِ يَدَيۡهِ وَمِنۡ خَلۡفِهِۦ يَحۡفَظُونَهُۥ مِنۡ أَمۡرِ ٱللَّهِۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُغَيِّرُ مَا بِقَوۡمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُواْ مَا بِأَنفُسِهِمۡۗ وَإِذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِقَوۡمٖ سُوٓءٗا فَلَا مَرَدَّ لَهُۥۚ وَمَا لَهُم مِّن دُونِهِۦ مِن وَالٍ

Na Mwenyezi Mungu Anayetukuka Ana Malaika wanaompitia binadamu, kundi baada ya kundi, mbele yake na nyuma yake, wanamhifadhi kwa amri ya Mwenyezi Mungu na kuyadhibiti yanayofanywa na yeye, mema au maovu. Hakika Mwenyezi Mungu , Aliyetakata na kutukuka, Hageuzi neema aliyowaneemesha watu mpaka wakiwa wao watayageuza yale waliyoamrishwa na Mola wao na wakamuasi. Na Mwenyezi Mungu Akiwatakia watu mitihani basi hakuna namna ya kuyakimbia, na hawana wao asiyekuwa Mwenyezi Mungu msimamizi yoyote wa kuyasimamia mambo yao, akawaletea yanayopendwa na akawakinga na yanayochukiwa. info
التفاسير:

external-link copy
12 : 13

هُوَ ٱلَّذِي يُرِيكُمُ ٱلۡبَرۡقَ خَوۡفٗا وَطَمَعٗا وَيُنشِئُ ٱلسَّحَابَ ٱلثِّقَالَ

Yeye Ndiye Ambaye anawaonesha umeme, nao ni mwangaza unaong’aa kutoka ndani ya mawingu, mkawa mnaogopa msishukiwe na vimondo venye kuchoma kutokana na umeme huo, na pia mkawa mnatazamia mvua inyeshe. Na kwa uweza Wake, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, anayleta mawingu yanayobebeshwa maji mengi kwa ajili ya manufaa yenu. info
التفاسير:

external-link copy
13 : 13

وَيُسَبِّحُ ٱلرَّعۡدُ بِحَمۡدِهِۦ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ مِنۡ خِيفَتِهِۦ وَيُرۡسِلُ ٱلصَّوَٰعِقَ فَيُصِيبُ بِهَا مَن يَشَآءُ وَهُمۡ يُجَٰدِلُونَ فِي ٱللَّهِ وَهُوَ شَدِيدُ ٱلۡمِحَالِ

Na radi linamtakasia Mwenyezi Mungu sifa Zake njema, matakaso yanayoonyesha dalili kwamba linamnyenyekea Mola Wake. Na Malaika wanamwepusha Mola wao na kila la upungufu kwa kumuogopa kwao Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu Anatuma vimondo vyenye kuangamiza, Akawaangamiza kwavyo anaowataka kati ya viumbe vyake. Na makafiri wanabisha juu ya upweke wa Mwenyezi Mungu na uweza Wake kufufufua, na hali Yeye Ana uweza mwingi na nguvu na ujabari wa kuwatesa waliomuasi. info
التفاسير: