ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್

ಪುಟ ಸಂಖ್ಯೆ:close

external-link copy
80 : 4

مَّن يُطِعِ ٱلرَّسُولَ فَقَدۡ أَطَاعَ ٱللَّهَۖ وَمَن تَوَلَّىٰ فَمَآ أَرۡسَلۡنَٰكَ عَلَيۡهِمۡ حَفِيظٗا

Yoyote mwenye kumkubali Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, na akafuata uongofu wake kivitendo, basi amemkubali Mwenyezi mungu Aliyetukuka na amefuata amri Yake. Na yoyote aliyekataa kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, basi hatukukutumiliza, ewe Mtume, kwa hawa wenye kukataa uwe ni mtunzi wa kuyadhibiti matendo yao na kuwahesabu kwa hayo. Hesabu yao ni juu yetu. info
التفاسير:

external-link copy
81 : 4

وَيَقُولُونَ طَاعَةٞ فَإِذَا بَرَزُواْ مِنۡ عِندِكَ بَيَّتَ طَآئِفَةٞ مِّنۡهُمۡ غَيۡرَ ٱلَّذِي تَقُولُۖ وَٱللَّهُ يَكۡتُبُ مَا يُبَيِّتُونَۖ فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ وَكِيلًا

Na hawa wenye kukataa, wakiwa kwenye baraza ya Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, wanajidhihirisha kuwa wanamtii Mtume na kuyafuata yale aliyokuja nayo, na wakiwa mbali na yeye na wakaondoka kwenye baraza yake, linatoka kundi katika wao likapanga njama kinyume cha yale waliyoyadhihirisha ya kumtii. Na wao hawakujua kwamba Mwenyezi Mungu Anadhibiti hesabu ya yale wanayoyapanga na kwamba Yeye Atawalipa kwa hayo malipo kamili. Basi wape mgongo na usiwajali, kwani wao hawatakudhuru. Na tegemea kwa Mwenyezi Mungu, kwani yeye Peke Yake Ndiye Mwenye kukutosha kwa usimamizi na utetezi. info
التفاسير:

external-link copy
82 : 4

أَفَلَا يَتَدَبَّرُونَ ٱلۡقُرۡءَانَۚ وَلَوۡ كَانَ مِنۡ عِندِ غَيۡرِ ٱللَّهِ لَوَجَدُواْ فِيهِ ٱخۡتِلَٰفٗا كَثِيرٗا

Kwani hawa hawaiangalii Qur’ani na haki iliyokuja nayo, kwa kuitaamali na kuizingatia, namna ilivyokuja kwa utaratibu uliopangika unaomfanya mtu awe na yakini kuwa inatoka kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake? Na lau yalikuwa yatoka kwa asiyekuwa Yeye, wangalipata ndani yake tafauti kubwa. info
التفاسير:

external-link copy
83 : 4

وَإِذَا جَآءَهُمۡ أَمۡرٞ مِّنَ ٱلۡأَمۡنِ أَوِ ٱلۡخَوۡفِ أَذَاعُواْ بِهِۦۖ وَلَوۡ رَدُّوهُ إِلَى ٱلرَّسُولِ وَإِلَىٰٓ أُوْلِي ٱلۡأَمۡرِ مِنۡهُمۡ لَعَلِمَهُ ٱلَّذِينَ يَسۡتَنۢبِطُونَهُۥ مِنۡهُمۡۗ وَلَوۡلَا فَضۡلُ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ وَرَحۡمَتُهُۥ لَٱتَّبَعۡتُمُ ٱلشَّيۡطَٰنَ إِلَّا قَلِيلٗا

Na likiwajia, hawa ambao Imani haijakita ndani ya nyoyo zao, jambo ambalo inapasa lifichwe linalofungamana na usalama, ambao heri yake itarudi kwa Uislamu na Waislamu, au hofu, ambayo inatia babaiko ndani ya nyoyo zao, wanalitoa nje na kulitangaza kwa watu. Na lau wao walilipeleka, lile liliowajia, kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye na kwa wenye ujuzi na ufahamu, wangaliujua uhakika wake wale wachambuzi kati yao. Na lau si Mwenyezi Mungu kuwafanyia wema na kuwaonea huruma, Mungalimfuata Shetani na mawazo mnayotiwa naye, isipokuwa wachache katika nyinyi. info
التفاسير:

external-link copy
84 : 4

فَقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا تُكَلَّفُ إِلَّا نَفۡسَكَۚ وَحَرِّضِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَكُفَّ بَأۡسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ وَٱللَّهُ أَشَدُّ بَأۡسٗا وَأَشَدُّ تَنكِيلٗا

Basi pigana jihadi, ewe Nabii, katika njia ya Mwenyezi Mungu na kulitukuza neno Lake. Hulazimishwi kitendo cha asiyekuwa wewe wala hutaadhibiwa kwacho. Na wahimize Waumini kupigana jihadi na uwavutie wafanye hivyo, kwani huenda Mwenyezi Mungu Akazuia, kwa ajili yako na wao, mashambulizi ya makafiri na nguvu zao. Na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ana nguvu nyingi zaidi na Ana adhabu kubwa zaidi kwa makafiri. info
التفاسير:

external-link copy
85 : 4

مَّن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةً حَسَنَةٗ يَكُن لَّهُۥ نَصِيبٞ مِّنۡهَاۖ وَمَن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةٗ سَيِّئَةٗ يَكُن لَّهُۥ كِفۡلٞ مِّنۡهَاۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ مُّقِيتٗا

Mwenye kumshughulikia mwingine apate mema, atapata fungu la thawabu kwa huko kuingilila kwake kati. Na mwenye kujishughulisha juu ya kumdhuru mwingine, Atapata fungu la mzigo wa dhambi. Na Mwenyezi Mungu ni Shahidi na ni Mtunzi wa kila jambo. info
التفاسير:

external-link copy
86 : 4

وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٖ فَحَيُّواْ بِأَحۡسَنَ مِنۡهَآ أَوۡ رُدُّوهَآۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٍ حَسِيبًا

Na Muislamu akiwatolea salamu, muitikieni kwa maneno mazuri zaidi na kwa furaha zaidi, au muitikieni salamu kama vile alivyowatolea. Na kila mmoja ana thawabu zake na malipo yake. Hakika Mwenyezi Mungu Aliyetukuka ni Mwneye kulipa kwa kila kitu (mnachokifanya). info
التفاسير: