ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್

ಪುಟ ಸಂಖ್ಯೆ:close

external-link copy
22 : 39

أَفَمَن شَرَحَ ٱللَّهُ صَدۡرَهُۥ لِلۡإِسۡلَٰمِ فَهُوَ عَلَىٰ نُورٖ مِّن رَّبِّهِۦۚ فَوَيۡلٞ لِّلۡقَٰسِيَةِ قُلُوبُهُم مِّن ذِكۡرِ ٱللَّهِۚ أُوْلَٰٓئِكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

Je, yule ambaye Mwenyezi Mungu Amemkunjua kifua chake, akabahatika kuukubali Uislamu, kuufuata na kuuamini, akawa yuko kwenye uwazi wa jambo lake na uongofu kutoka kwa Mola wake, je ni kama yule ambaye hayuko hivyo? Hao wawili hawalingani. Basi ole wao na maangamivu wale ambao nyoyo zao zilikuwa ngumu na zikajiepusha na utajo wa Mwenyezi Mungu. Hao wako kwenye upotevu ulio kando na haki waziwazi. info
التفاسير:

external-link copy
23 : 39

ٱللَّهُ نَزَّلَ أَحۡسَنَ ٱلۡحَدِيثِ كِتَٰبٗا مُّتَشَٰبِهٗا مَّثَانِيَ تَقۡشَعِرُّ مِنۡهُ جُلُودُ ٱلَّذِينَ يَخۡشَوۡنَ رَبَّهُمۡ ثُمَّ تَلِينُ جُلُودُهُمۡ وَقُلُوبُهُمۡ إِلَىٰ ذِكۡرِ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ هُدَى ٱللَّهِ يَهۡدِي بِهِۦ مَن يَشَآءُۚ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَمَا لَهُۥ مِنۡ هَادٍ

Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Aliteremsha Mazungumzo mazuri zaidi kuliko yote, nayo ni Qur’ani tukufu, inayofanana katika uzuri wake, upangikaji wake na kutotafautiana kwake, ndani yake mna hadithi, hukumu, hoja na dalili zilizo wazi. Kusomwa kwake kunarudiwa na ule wingi wa kuikariri hauifanyi ichokeshe. Isomwapo huifanya miili ya wenye kuisikia itetemeke na zitikisike ngozi za wale wanaomuogopa Mola wao, kwa kuathirika na yale yaliyomo ndani yake ya kutisha na kuonya, kisha zikalainika ngozi zao na nyoyo zao kwa kufurahia bishara iliyomo ya ahadi njema na mahimizo ya kufanya kheri. Kuathirika huko na Qur’ani ni uongofu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa waja Wake. Na yoyote yule ambaye Mwenyezi Mungu Anayempoteza asiiamini hii Qur’ani kwa sababu ya ukafiri wake na ushindani wake, basi hana muongozi mwenye kumuongoa na kumuafikia. info
التفاسير:

external-link copy
24 : 39

أَفَمَن يَتَّقِي بِوَجۡهِهِۦ سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ وَقِيلَ لِلظَّٰلِمِينَ ذُوقُواْ مَا كُنتُمۡ تَكۡسِبُونَ

Je, Yule atakayetupwa Motoni akiwa amefungwa, akawa hawezi kujikinga na Moto isipokuwa kwa uso wake, kwa ukafiri wake na upotevu wake, ni bora au ni yule anayestarehe Peponi, kwa kuwa Mwenyezi Mungu Amemuongoa? Na madhalimu Siku hiyo wataambiwa, «Onjeni madhara ya yale mliokuwa mkiyachuma duniani ya kumuasi Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
25 : 39

كَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ فَأَتَىٰهُمُ ٱلۡعَذَابُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَشۡعُرُونَ

Wale waliokuwa kabla ya watu wako, ewe Mtume, waliwakanusha Mitume wao, hivyo basi adhabu ikawajia kwa namna ambayo hawakuhisi kuja kwake. info
التفاسير:

external-link copy
26 : 39

فَأَذَاقَهُمُ ٱللَّهُ ٱلۡخِزۡيَ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Basi Mwenyezi Mungu Akawaonjesha ummah waliokanusha adhabu na unyonge duniani, na Akawaandalia adhabu kali zaidi na ngumu zaidi huko Akhera. Lau hawa washirikina wangalijua, kuwa kile kilichowashukia ni kwa sababu ya ukafiri wao na ukanushaji wao, wangaliwaidhika. info
التفاسير:

external-link copy
27 : 39

وَلَقَدۡ ضَرَبۡنَا لِلنَّاسِ فِي هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ مِن كُلِّ مَثَلٖ لَّعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Na kwa hakika tumewapigia hawa wenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu kila mfano katika mifano ya watu wa kame zilizopita, kwa kuwatisha na kuwaonya, ili wakumbuke na wakomeke na lile ambalo wako nalo la kumkufuru Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
28 : 39

قُرۡءَانًا عَرَبِيًّا غَيۡرَ ذِي عِوَجٖ لَّعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ

Na tumeijaalia hii Qur’ani ni kwa lugha ya Kiarabu, yenye matamshi yaliyofunuka wazi na yenye maana mepesi yasiyo na uchanganyifu wala upotofu, huenda wao wakamcha Mwenyezi Mungu kwa kufuata amri Zake na kuepuka makatazo yake. info
التفاسير:

external-link copy
29 : 39

ضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا رَّجُلٗا فِيهِ شُرَكَآءُ مُتَشَٰكِسُونَ وَرَجُلٗا سَلَمٗا لِّرَجُلٍ هَلۡ يَسۡتَوِيَانِ مَثَلًاۚ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Mwenyezi Mungu Anapiga mfano wa mtumwa aliyemilikiwa na washirika wenye kuteta, na mtumwa mwingine aliyekuwa ni wa mmiliki mmoja tu, akawa yuwajua matakwa yake na yanayomridhisha. Je, mfano wa wawili hao unalingana? Basi Hivyo ndivo alivyo mshirikina. Yeye yuko katika hali ya mshangao na shaka, na Muumini yuko katika raha na utulivu. Sifa njema kamilifu zilizotimia ni za Mwenyezi Mungu, Peke Yake, lakini washirikina hawaijui haki wakaifuata. info
التفاسير:

external-link copy
30 : 39

إِنَّكَ مَيِّتٞ وَإِنَّهُم مَّيِّتُونَ

Wewe ni mwenye kufa, ewe Mtume, na wao ni wenye kufa, info
التفاسير:

external-link copy
31 : 39

ثُمَّ إِنَّكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ عِندَ رَبِّكُمۡ تَخۡتَصِمُونَ

kisha nyote, Siku ya Kiyama. Kwa Mola wenu mtagombana, hapo Ahukumu baina yenu kwa uadilifu na usawa. info
التفاسير: